SIRI TATU ZINAZOWEZA KULETA USHINDI MKUBWA.
--------------------------------------------------------------------------
Na, Steven Mshiu.
Shalom mtu mwema sana wa Mungu. Naamini umekuwa na wakati mwema wa
mapumziko mazuri ya kuikumbuka pasaka ambayo Yesu alitolewa au alijitoa
kwa ushindi mkubwa ili kuleta ukombombozi wa mwanadamu.
Tunapoadhimisha siku hii tukumbuke kuwa Yesu yu karibu kurudi kulichukua
kanisa au wale watakaokuwa na alama ya damu ya Yesu ktk mioyo yao. Damu
iliyotuletea wokovu mkuu sana.
Jana niliweza kupata fursa na kibali
cha kufundisha Neno la Mungu katika kanisani, hapa moshi-Mdawi, na
niliweza kushirikiana ujumbe huu ambao ulikuwa baraka sana kwangu
binafsi na hata kwa washirika wote.
Hivyo nimeona ni vyema nikakushirikisha nawe japo kwa kidogo tu.
Unafahamu kuwa hakuna ushindi unaopatikana kimiujiza ujiza. Hakuna
ushindi unaotokea from nowhere. Ushindi unapatikana kwa kuvuja jasho,
tena baada ya maumivu makubwa sana.
Matokeo ya ushindi ni kutuzwa.
ILi mshindani aweze kutuzwa ni lazima ahakikishe anapambana hadi mwisho
wa mchezo. Huwezi kuishia katikati ya mchezo halafu ukategemea kupewa
zawadi. Hiyo itakuwa ni ndoto.
Yapo mambo mengi yanayoweza kuwa
sababu ya kukuletea ushindi mkubwa sana, lakini kwa leo nataka nikuletee
mambo haya matatu ambayo yamekuwa ni siri kubwa na yenye mafaniko kwa
washindani.
#SiriYaKwanza.
UJASIRI. Unapoingia katika mashindano yoyote yale jambo la kwanza
unalotakiwa kufanya ni kujivika ujasiri. Ujasiri ni kile kitendo cha
kufanya jambo pasipo kuwa na woga, pasipo kuwa na hofu. Huku ukitarajia
kuwa kuna matokeo mazuri yatakayotokea juu ya kile unachokifanya.
Ujasiri unakupa uwezo wa kujiamini.
Ujasiri unakufanya umuone
mshindani wako kuwa hana uwezo kama wako. Kwa wale mashabiki wa mpira
wanaweza kukubaliana nami, maana timu zinapoingia uwanjani huingia kwa
ujasiri mkubwa sana huku kila timu ikiamini kuwa ni lazima ishinde.
Kifo cha msalaba kilihitaji mtu jasiri. Mtu atakaekubali kudharauliwa na
kuaibishwa kwa ajili ya makosa ya wanadamu. UJASIRI ndio kitu pekee
kilichoweza kumfanya YESU aiistahimili hukumu ya kifo cha msalaba. Kitu
kinachohafifisha Ujasiri ni maneno ya watu. Dharau kutoka kwa
wanaokuzunguka. Unaweza ukapanga kufanya jambo fulani either biashara,
lakini watu wanapoanza kukubeza na kukudharau ile hali ya kuthubutu
inapotea na hatimaye unaingia katika hatari ya kulipoteza lengo na
kusudi la wewe kuishi hapa duniani.
#SiriYaPili. KUSUDI KAMILI.
Hakuna mwanadamu aliezaliwa kwa bahati mbaya. Kila mwanadamu yupo hapa
duniani kwa kusudi maalum. Katika dunia hii ya sasa yenye ushindani
mkubwa kila nyanja inahitaji watu wenye kulitumika kusudi lao la kuwepo
hai hadi wakati huu. Unapolitambua kusudi kamili ni lazima mabadiliko
yatokee. Yesu alilitambua kusudi lake la kuja hapa duniani baada ya
kuacha kila kitu huko mbinguni. Kusudi kuu lilikuwa ni kumwokoa na
kumkomboa mwanadamu. Na hakukubali kuondoka hapa duniani kabla ya
kulitimiza kusudi hilo.
Nawe pia unalo kusudi. Je utaondoka hapa
duniani kabla hujalitimiza? Kumbuka kusudi kubwa la kuokolewa kwetu ni
ili tumtumikie Mungu kama Yesu anavyotuagiza ktk Mathayo 28:18-20.
Baada ya utumishi huo thawabu yake inapatikana ktk Yohana 14 na 15.
Mpendwa litumike kusudi hili. Tupo kwenye mashindano. Mpambano wetu ni
juu ya shetani anaeibeza kazi ya msalaba. Ni lazima tupambane na
tuhakikishe tunamshinda. Na tutapambana nae kwa kuitangaza habari Ya
Msalaba. Habari za mshindi Yesu. Kwa kuwa Yesu alishinda Nasi tutashinda
tu. KUSUDI KAMILI.
#SiriYaTatu. IMANI
Imani ni jambo kubwa sana na ni kitu cha muhimu kwa mwanadamu yeyote.
Kila jambo linalofanyika na kuleta matokeo makubwa huanza kwa imani.
Mkulima analima shamba, hakuna dalili yeyote ile ya mvua. Anaotesha
mbegu ardhini tena kwenye vumbi. Imani yake kubwa ni kwamba mvua
itanyesha na zile mbegu zitaoza na kuota na hatimae kuleta mavuno mengi.
Mtu anaanza biashara kwa mtaji wa 50,000/= lakini anaamini kuwa kuna
siku mtaji wake utakuwa mkubwa naatamiliki biashara kubwa. Tunawasiliana
Na Mungu kupitia maombi ya imani. Imani anatufanya tuamini kuwa Mungu
yupo. Tunaokolewa kwa imani tu, Imani yetu inatufanya tukubaliane na
yale yote aliyotuagiza Yesu. Tunaamini kuwa kuna Makao ambayo
yameandaliwa huko mbinguni kwa wale watakaoshinda. Imani Imani Imani.
Yonathani mtoto wa Mfalme Sauli alitumia siri hizi katika kitabu cha 1
Samwel 14:1-16. Aliweza kuwaletea Israeli ushindi mkubwa sana.
Jambo
la msingi ni kuamini kuwa Mungu yupo pamoja nawe kwa kila unalolifanya
kwa ajili ya kulitimiza kusudi. Na yuko tayari kukupatia ushindi mkubwa
sana utakaokuwa historia kwa wale wanaokubeza.
Mungu akubariki sana.
(kesho nitakuletea sababu zinaokwamisha au kuchelewesha ushindi na namna ya kuzishinda)
@Steven Mshiu.
0655-882074
smshiu42@gmail.com
Jumatano, 19 Aprili 2017
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
MAKUNDI MAWILI YA WATU WANAOKUZUNGUKA.
FAHAMU MAKUNDI MAWILI YA WATU KATIKA MAISHA YAKO. Na Steven Mshiu . Maisha ya kila mwanadamu yamezungukwa na watu. Watu hawa waweza kat...
-
KUNA HAJA YA KANISA KUOMBA KWA AJILI YA VIJANA Na Steven Mshiu. Siku mbili zilizopita nikiwa katika tafakari yangu binafsi juu ya musta...
-
UNAJUA MAHALI SAHIHI PA KUWEKA TUMAINI LAKO? Na Steven Mshiu, Habari mpenzi msomaji wa makala zangu. Ni matumaini yangu u bukhe...
-
NGUVU YA USHUHUDA. Na Steven Mshiu. Habari za leo mpendwa rafiki. Naamini una uzima wa kutosha kabisa. Ni jambo la kumshukuru Mungu san...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni