KULEWA MADARAKA.
Na, Steven Mshiu
Leo napenda tuangalie hili suala la madaraka.
Madaraka ni mfumo wa Mungu mwenyewe aliounzisha huko mbinguni yeye
mwenyewe. Mungu yeye mwenyewe mi mwenye madaraka na hufuata protoko
yaani husimamia kanuni zake za kiuongozi na utawala.
Kiongozi yeyote
anaesimama na kuliongoza taifa lolote, hupewa mamlaka na maongozi
kutoka kwa Mungu. Hivyo ni vyema kuitii na kuiheshimu kila mamlaka
iliyopo. Sisi hatuna mamlaka ya kumhukumu kiongozi yeyote anaesimama
mbele yetu hata kama amekosea kiasi gani. Yupo Mungu aliemuweka ndiye
anaeweza kumhukumu. Biblia inatuagiza hivyo.
Leo nataka nikuletee
kisa kimoja cha mtu alieitwa Sauli. Sauli alichaguliwa na kutawazwa na
Mungu ili awe mfalme juu ya taifa la Israel. Mtu huyu alitoka ktk jamii
ndogo sana ya Israel yaani alikuwa ni jamaa ya Benyamini.
Baada ya
wana wa Israel kukosa mfalme na mwamuzi juu yao kwa muda mrefu sana
tangu kipindi cha Samsoni ndipo wakamwambia Samwel awatafutie mfalme
atakaewaongoza ktk vita. Nyakati hizo taifa hili teule la Mungu lilikuwa
limemsahau Mungu kabisa. Hawakutambua mamlaka na madaraka ya Mungu kuwa
ni tofauti na ya dunia hii
Hawakukumbuka aliewaongoza jangwani pindi walipotoka Misri. Hivyo wakawa wanataka mfalme. Ndipo Mungu alipomwinua Sauli.
Baada ya Sauli kuinuliwa na kuwa mfalme juu ya Israel, akaota pembe.
Akajisahau ya kwamba ametoka ktk jamii ndogo sana ya Benyamini. Akasahau
kuwa alipakwa mafuta illi aliamue taifa teule la Mungu. Akaacha
kumsikiliza mchungaji wake Samwel. Akajipa cheo cha Mungu. Akajiona kama
yeye ni mungu wa israel. Akafanya kama alivyoweza.
Siku moja
Bwana Mungu akampa Samweli maelekezo kuwa amwambie Sauli aende awapige
Amaleki na kuharibu kabisa kila kitu cha hao Amaleki maana waliwatesa
sana Israel walipokuwa wakitoka Misri. Tena asiache mfugo hata mmoja wa
hawa Waamaleki.
Sauli hakutaka kuyasikia hayo maneno na maagizo ya Mungu kupitia kwa Samwel.
Sauli akatoka akaandaa jeshi kuishukia Amaleki. Akajifanya mwema sana.
Akawaambia Wakeni waliokaa Amaleki kuwa waondoke asije akawaua pamoja na
Amaleki. Akaanza kuipiga Amaleki. Akawaona kondoo na ng'ombe walionona
akawaacha. Akamkamata mfalme Agagi, mfalme wa Waamaleki na kumwacha hai.
Lakini mtu huyu alipewa maagizo kuwa asiache kitu hata kidogo. Wala hakuyatii maagizo hayo. Akafanya kwa maamuzi yake.
Mungu akanena na Samweli kwa mara nyingine kuwa anajuta kwa sababu
alimtawaza ili awe mfalme maana amerudi nyuma wala asimfute Mungu. Wala
hakufanya yale aliyomwamuru. Kwa hiyo Mungu akamkataa kabisa Sauli. Ni
kwa sababu alilewa madaraka.
Sauli alipoulizwa kwanini hakutii
maagizo ya Mungu, yeye alijitetea kuwa ametii na amewachukua hao wanyama
ili waje kumtolea Mungu sadaka. Mara ni wale watu ndio waliowaacha hao
kondoo. Yeye hakusimama ktk nafasi yake. Hakuambiwa amwache Agagi akiwa
hai. Hili likawa ni kosa kubwa sana mbele za Mungu.
Hivyo Mungu akamwacha Sauli kabisa. Tena akamkataa. Yote haya ni kwa sababu alilewa madaraka.
Siku za leo kuna watu ambao Mungu amewadhamini na kuwapa kanafasi
kadogo tu ka uongozi lakini wanautumia vibaya. Kumbuka uko kwa niaba ya
Mungu. Tumia mamlaka yako vizuri. Watendee wananchi haki. Tafuta
kuyafuata maagizo ya Mungu. Viongozi wa dini wana nafasi kubwa sana ktk
nafasi yako ya uongozi. Ni vyema kuwasikiliza. Wao ni sauti ya Mungu.
Wao ndio kina Samwel wa leo. Ndipo utakapoona mafanikio makubwa ktk
mamlaka uliyopewa.
Kisa hiki sio mimi niliyetunga. Ni maandiko
halisi kutoka katika Biblia. Kisa hiki kwa wale wasomaji wa Biblia
kinapatikana ktk kitabu cha 1 Samwel 15:1-34.
Tumia nafasi unayoipata kwa umakini.
Mungu akubariki sana.
0655 882074
Jumatano, 19 Aprili 2017
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
MAKUNDI MAWILI YA WATU WANAOKUZUNGUKA.
FAHAMU MAKUNDI MAWILI YA WATU KATIKA MAISHA YAKO. Na Steven Mshiu . Maisha ya kila mwanadamu yamezungukwa na watu. Watu hawa waweza kat...
-
KUNA HAJA YA KANISA KUOMBA KWA AJILI YA VIJANA Na Steven Mshiu. Siku mbili zilizopita nikiwa katika tafakari yangu binafsi juu ya musta...
-
UNAJUA MAHALI SAHIHI PA KUWEKA TUMAINI LAKO? Na Steven Mshiu, Habari mpenzi msomaji wa makala zangu. Ni matumaini yangu u bukhe...
-
NGUVU YA USHUHUDA. Na Steven Mshiu. Habari za leo mpendwa rafiki. Naamini una uzima wa kutosha kabisa. Ni jambo la kumshukuru Mungu san...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni