Jumatano, 28 Juni 2017

Matokeo Mabovu ya Kutotii Sauti ya Mungu



MATOKEO MABOVU YA KUTOTII SAUTI YA MUNGU.
Na Steven MshiuMara nyingi Mungu huwa anasema na mtu au watu kabla hajafanya jambo fulani. Hii inategemea wewe umejiweka ktk nafasi gani ya kuweza kumsikia wakati akinena. Tumejikuta tukikwama kutokana na kutokuelewa kwetu kuwa Mungu anasema nasi kitu gani.
Wakati Eli alipotoka nje ya kusudi la Mungu, akafanya kama alivyoweza ndani ya hekalu, akaacha kuwalea watoto wake ktk maadili ya kiroho, wakalichezea hekalu la Mungu, wakafanya dhambi na uchafu wa kila namna kama walivyoweza bila kuulizwa chochote na baba yao Eli. Ndipo hasira ya Bwana ilipowaka juu ya Eli na wanawe. Mungu akaacha kuongea na Eli, kwa sababu hakuwa anayafuata maagizo yake tena. Na wakati huu neno la Mungu lilikuwa adimu sana ktk Israel. Kwa sababu bado Mungu alikuwa analipenda taifa la Israel, ndipo alipoanza mpamgo wa kumtafuta na kumwandaa Samwel kuichukua nafasi ya Eli. 1 samwel 2:35, Sikio la kufa siku zote huwa halisikii dawa. licha ya unabii wote huu bado Eli hakuweza kutubu wala kufanya juhudi za kulirejeza hekalu na taifa ktk hali ya utakatifu wa Mungu.
Mungu anaposema na Samwel juu ya dhambi ya Eli, anaanza kumwambia yatakayompata Eli pamoja na familia yake. 1 Samwel 3:11-14. Tayari Mungu alishamkataa moja kwa moja. Hapa anasema mambo makubwa na mabaya yatakayompata Eli na familia yake. Hakuna kitu kibaya kama kukataliwa na Mungu. Mungu anapokukataa kifo ni lazima kiwe nyuma yako. Na hatua ya kwanza unaanza kudhoofika kiroho. Kifo cha kimwili kama kinavyoonekana ktk 1 Sam 4:11,19 ni matokeo ya kifo cha kiroho.
Jambo lingine ni utukufu wa Mungu kuondoka. Mungu anakaa pale ambapo utakatifu wake unaenziwa. mahali ambapo anaposema watu wanaisikia sauti yake. Lakini wakati dhambi inapoingia tu basi utukufu wake huondoka. 1 Sam 5:1-2.
Yapo matokeo meeengi yanayotokana na kutoitii sauti ya Mungu. Kuna wakati hata wewe Mungu alisema nawe kuhusu kufanya jambo fulani, na unaweza ukawa ni shahidi wa kilichotokea kama ulitekeleza au la. Ni vizuri kutii na kufanya kile anachotuagiza Mungu ili aendelee kuwa pamoja nasi. Yeye anampenda mtu mti na mnyenyekevu anaeisikia sauti yake na kufuata maagizo yake.
Naibariki asubuhi yako na Mungu awe pamoja nawe kwa kila unalolifanya linalomletea utukufu.
Steven Mshiu
+255 655 882074
+255 768 882074
smshiu42@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MAKUNDI MAWILI YA WATU WANAOKUZUNGUKA.

FAHAMU MAKUNDI MAWILI YA WATU KATIKA MAISHA YAKO. Na Steven Mshiu . Maisha ya kila mwanadamu yamezungukwa na watu. Watu hawa waweza kat...