Jumatano, 28 Juni 2017

MTAZAMO WA MUNGU NA MTAZAMO WA WANADAMU



MTAZAMO WA MUNGU NA MTAZAMO WA WANADAMU.
------------------------------------------------------------------
Na, Steven Mshiu
Nakusalimu kupitia jina la Kristo Yesu ambaye ni Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Ni matumaini yangu kuwa bado una uzima wa kutosha. Nina kila sababu ya kumtukuza Mungu kwa hilo.
Tumekuwa busy sana kwa mambo
mbalimbali, hadi kukosa muda wa kuweza kuweka
makala katika blog hii, ni kwa sababu tunaandaa mipango mizuri ya kuhakikisha blog hii inakuwa bora zaidi. Tumeshapata walimu kadhaa wa Neno la Mungu, na mapema tu utajifunza mengi, utahamasika kwa mengi kupitia blog hii. Lengo letu ni kuihubiri injili ya Kristo inayoleta wokovu kwa wanadamu. Ndicho kiini cha blog hii.
Leo napenda nikuletee makala hii fupi. Nafikiri
itakuhamasisha na kukupa morali wa kuamini kuwa kile Mungu alichokisema
juu ya maisha yako ni lazima kitimie haijalishi ni kwa muda gani. Unajua wanadamu tuna mtazamo, na Mungu pia ana mtazamo. Wewe waweza kuona hivi, Mungu akaona vile. Hivyo kuna tofauti kubwa sana kati ya mtazamo wa MUNGU na wa wanadamu.
Nikuletee kisa kimoja kwa leo ndani ya Biblia kinachomhusu mmoja wa watoto wa YAKOBO mwana wa ISAKA Ambaye ni uzao wa ahadi ya MUNGU kwa IBRAHIMU. Alikuwa ni mtoto wa 11 katika uzao wa Yakobo na kifungua mimba katika tumbo la Rahel, nduguye Leah. Kumbuka Isaka alikuwa na wake wawili (Lea na Rahel). Jina lake aliitwa YUSUFU.
Yusufu alikuwa ni mwana wa uzee kwa Yakobo, hivyo kwa kiswahili chepesi, baba yake alimdekeza sana, kama yeye(babaye)
alivyodekezwa na mamaye Rebeka.
 Mtazamo wa Yakobo kwa Yusufu alimtazama kama mpelelezi wa
nduguze, maana kipindi fulani alikuwa akienda kuwatazama nduguze makondeni
na kumletea babaye habari. Mwanzo 37:2-3.
Kwa ndugu zake, mtazamo wa ndugu zake Yusufu, walimtazama kama ni kiherehere, mmbea na mnafiki, hivyo wakamchukia Mwanzo 37:4 Haikuishia hapo.
Waishmaili wakamtazama Yusufu kwa mtazamo wa kibiashara. Hivyo wakamnunua Yusufu, Mwanzo 37:27-28 Kwa kuwa wa- Ishmaili walikuwa ni wafanyabiashara, na wameshapata dili jepesi hivyo wakamuuza tena kwa wafanyabiashara wengine wakubwa ambao ni wa-Midian. Na wa-Midian nao wakamuuza tena kwa POTIFA.
N.B: Kumbuka hii ni mitazamo ya wanadamu juu ya YUSUFU, Lakini Mungu alishamtazama kivingine, hivyo kote huku anakopitia mtazamo wa Mungu uko pale pale. Kwa Potifa. Potifa akamtazama YUSUFU kama mlinzi wa nyumba yake maana alikuwa mwaminifu sana. Mwanzo 39:4-5 Lakini bado mitizamo ya wanadamu haiishi. Mke wa POTIFA akamtazama kwa mtaza.mo wa tamaa. Yaani mtazamo wa kimapenzi, kwa kuwa alikuwa ni kijana mzuri, body yake iko safi. Hivyo akamtamani Mwanzo 39:6b-7. Na kwa sababu kijana huyu asieijua dhambi alikuwa akilinda utakatifu wake na mtazamo wa MUNGU kwake, hivyo hakutenda dhambi yoyote.
Katika kukimbia kwake akaangukia gerezani, mle gerezani wakamtazama kama ni mhalifu mkubwa sana. Maana alifungwa katika gereza la mfalme. Mwanzo 39:20, Mkuu wa gereza naye akamtazama Yusufu
kama msimamizi wa wenzake 39:21 Wakati wa MUNGU kudhihirisha jinsi anavyomtazama YUSUFU ulipofika, hakuna hata mmoja alieweza kuubadilisha.
Akiwa gerezani, ndipo mtazamo wa Mungu ulipoanzia safari ya kutimia. Miongoni mwa wafungwa wa mfalme, wawili wanaota ndoto, na Yusufu anawatafsiria. Kutokana na tafsiri ya Yusufu, yakawa ya kweli. Farao akaota ndoto ambayo ilimnyima usingizi na hapakupatikana mtu wa kuitafsiri.
Yule mfungwa mmoja akamkumbuka Yusufu alivyomtafsiria ile ndoto yake, akapeleka ombi kwa farao, kuwa kuna mfungwa/mhalifu mmoja wa kiebrania katika gereza la mfalme anaweza
kuitafsiri ndoto yako. Yusufu akaitwa mbele ya Farao na kuitafsiri ndoto. Hakika ikawa ni ya kweli.
Soma Mwanzo sura ya 41. Yusufu akapata kibali mbele ya Farao. Mwanzo 41:37-40. MUNGU
ALIMTAZAMA YUSUFU KAMA MTU WA TATU KTK TAIFA LA MISRI. Kwa lugha nyingine ni kwamba Mungu alimtazama
kama WAZIRI MKUU. (Mwanzo 41:41-42). Wakati wa kuinuliwa kwa Yusufu ukafika. Muda hautoshi kuendelea kuandika mengi, ila nina haya ya kuandika,
Wanadamu wanaweza
wakakutazama kama kahaba/malaya fulani hivi, lakini Mungu akakutazama kama mama/baba bora wa familia. Wanaweza wakakutazama kama
jambazi/mwizi fulani hivi lakini Mungu akakutazama kama mtumishi wake. Wanaweza wakakutazama mtumwa lakini Mungu akakutazama kama mfalme.
Wanaweza wakakutazama kama
asie na mwelekeo lakini Mungu akakutazama kama kiongozi mkubwa. Wanaweza wakakutazama kama masikini lakini Mungu akakutazama kama tajiri. Wanaweza wakakutazama kama
wewe ni wa kufa tu lakini Mungu akakutazama kama mtu wa kuishi. MTAZAMO WA MUNGU NI TOFAUTI KABISA NA MTAZAMO WA WANADAMU.
Walimtazama Daudi kama kijana mdogo, tena mchungaji wa kondoo tu, ambaye hayawani wanaweza kuila nyama yake. lakini Mungu alimtazama kama
shujaa na Mfalme wa Israel. Wanadamu wasikutishe na
mitizamo yao.
Nimalizie kwa kukumbusha mambo
machache.
*Ili mtazamo wa Mungu utimie ktk maisha yako ni lazima uuishi huo mtazamo. Mwanzo 39:9.
*Dhambi ni kikwazo kikubwa cha mtazamo wa Mungu kutimia. Amuzi 16:17-20
*Pale mtazamo wa Mungu unapotimia usilipe kisasi kwa wanadamu waliokuwa na mtazamo tofauti juu yako. Mwanzo 48:8-21
*Mtangaze Mungu wako kuwa yeye ndie mwezeshaji wa kila kitu.
Nikushukuru kwa kusoma ujumbe huu mfupi. Ni maombi yangu Mungu akakuinue na kutimiza kile alichoahidi katika maisha yako.
Ahsante.
Kama utakuwa na maoni au ushauri, unaweza kuwasiliana
na mwandishi wa makala hii,
Imeandikwa na Steven Mshiu,
0655-882074, 0768-882074
baruapepe smshiu42@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MAKUNDI MAWILI YA WATU WANAOKUZUNGUKA.

FAHAMU MAKUNDI MAWILI YA WATU KATIKA MAISHA YAKO. Na Steven Mshiu . Maisha ya kila mwanadamu yamezungukwa na watu. Watu hawa waweza kat...