Jumatano, 28 Juni 2017

Tumia Kipawa Mungu alichoweka Ndani Yako



TUMIA KIPAWA AMBACHO MUNGU AMEKIWEKA NDANI YA MOYO WAKO
 
Na Steven Mshiu .
Mungu anapoweka huduma au kipawa ndani ya moyo wako, yeye si mjinga. Anafahamu fika kuwa kuna mtu anaihitaji huduma yako au kile kitu ambacho Mungu ameweka ndani yako.
Nikiwa shuleni mwalimu wa Baiolojia aliwahi kunifundisha kitu kinachoitwa "use and disuse" Kwamba kadri kitu kinavyotumika sana ndivyo kinavyozidi kuwa imara, na endapo hakitatumika basi hupoteza ubora wake au kupotea kabisa.
Wakati nikienda shamba lile jembe ambalo nalitumia mara kwa mara linakuwa jepesi mkononi mwangu. Ni kwa sababu nimeshalizoea.
Mwanadamu anapozaliwa tayari Mungu alishaweka kazi maalum ndani yake. Yeremia anaambiwa kuwa atakuwa nabii na atakwenda kila mahali ambapo Mungu atamtuma. Yeremia anaanza kujitetea kuwa yeye bado ni mdogo.
Mungu anamwambia kuwa alimchagua tangu akiwa tumboni mwa mama yake kwa ajili ya kuharibu, kubomoa na kung'oa ili kupanda na kujenga.
Kwa hiyo hata wewe kuna kazi ambayo Mungu anataka uifanye. Mungu anampenda yule anayefanya kazi yake kwa kumtii yeye, kuyafuata maagizo yake ikiwa ni pamoja na kumtii yeye.
Unapofanya kazi ya Mungu kwa moyo na kwa kumtii yeye, yeye hufurahishwa na wewe.
Sauli mfal,e wa Israel, licha ya kuchaguliwa na Mungu kuwa mwamuzi wa Taifa la Israel baada ya Samwel, alijiona kuwa yeye hana muda wa kuyasikiliza maagizo ya Mungu kwani anaweza kufanya lolote kwa kuwa yeye ni Mfalme. Hata alipopewa maagizo ya kuwaua Amaleki wote yeye alimwacha Agagi Mfalme wa Amaleki angali hai.
Mungu akajuta kwanini alimchagua Sauli kuwa mfalme. Ni kwa sababu hakutaka kufuata maagizo ya Mungu katika kuitimiza kazi aliyoagizwa
Mwishowe Mungu alimkataa kabisa na kuuhamisha ule ufalme kutoka kwa Sauli na Kwenda kwa Daudi. Soma 1 Samweli 15
Yapo madhara yanayoweza kukupata endapo hutasimama katika nafasi Mungu aliyokuweka. Au pale ambapo utaacha kulifuata agizo la Mungu
Kwanza Mungu atajuta kwa ajili yako
Utaondolewa kwenye ile nafasi yako, na nafasi yako itapewa mtu mwingine
Mungu atakukataa kabisa
Sasa basi fanya mambo haya ili uendelee kubaki katika nafasi ambayo Mungu amekuweka
Mtii na kutekeleza kile Mungu anachokuagiza
Kuwa mnyenyekevu na mtu wa kujishusha
Usijikweze
Kuwa mtu wa kukubali kushauriwa(flexible)
Kuwa mvumilivu na mwenye subira
Kaa kwenye kusudi lako. Tekeleza kile unachotakiwa kukifanya
Tambua kuwa kuna watu wanaokutegemea ikiwa ni kujifunza kutoka kwako na mengine mengi.
Epuka kuwa m-binafsi. Kufanya mambo kwa kutegemea matakwa yako, kwa tamaa zako.
Kuwa mtu wa kujihukumu mwenyewe. yani mtu wa toba pale unapokuwa umekosea.
Ukifanya yote haya Mungu atajisifia kwa ajili yako kama alivyojisifia kwa Daudi kwamba Daudi ni mtu anaeupendeza moyo wa Mungu na anafuata kile anachomuagiza
Ahsante
Steven Mshiu
+255 655 882074
+255 768 882074
smshiu42@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MAKUNDI MAWILI YA WATU WANAOKUZUNGUKA.

FAHAMU MAKUNDI MAWILI YA WATU KATIKA MAISHA YAKO. Na Steven Mshiu . Maisha ya kila mwanadamu yamezungukwa na watu. Watu hawa waweza kat...