Jumatano, 28 Juni 2017

UNA NAFASI YA KUSTAWI TENA



USIKATISHWE TAMAA. BADO UNA NAFASI YA KUSITAWI TENA
---------------------------------------------------------------------------------------------------
Na, Steven Mshiu.
Shalom Mtu mwema wa Mungu. Ni faraja yangu kukuona ukisonga mbele bila kuhofia chochote. Nakutia moyo kuwa japo usiku umeendelea Sana asubuhi yako itafika tu.
Nimekuwa nikikutana na baadhi ya watu wakiniambia kuwa wamechoshwa na maisha eti yamekuwa magumu.
Juzi nikamuuliza mtu mmoja kuwa Kama maisha yamekuwa magumu hebu nipe "suggestion" yako tufanyeje?
Kweli hakuwa na jibu la kunipa kabisa. Nikamwambia. Mpendwa, Ukibaki kulalamika tu ni kweli utaona maisha kuwa ni magumu.
Lakini ukitambua kuwa wewe ni mwana wa Mungu Hakika utakula mema ya nchi.
Nikamwambia kuwa maua ya kondeni, Mungu huyavisha na kuyapendezesha. Kiasi kwamba mazungu wanaweza kutumia gharama nyingi tu kuja kuyaangalia.
Nikamkumbusha tena kuhusu ndege wa angani. Wao hakuna sehemu yoyote ile wamelima shamba lakini Mungu huwalisha kila siku.
Sasa kwako wewe mwanadamu uliyeumbwa na Mungu sio zaidi ya hawa ndege au maua??
Tunaishi kwenye dunia ambamo kuna vitu vingi vinavyokatisha tamaa, Hali ya kimaisha kuwa ngumu inaweza kukukatisha tamaa. Unaweza kujikuta umesoma na una vyeti safi lakini una miaka zaidi ya nane bado hujapata kazi. Kukosa kazi kukakufanya ukate tamaa kabisa na kujutia elimu yako.
Unaweza kuwa na wazo la kufanya jambo fulani na umejiandaa vyema lakini kwa kuwa kuna ambaye alishindwa jambo hilo anaamua kukukatisha tamaa, na wewe ukakubali kukatishwa tamaa. Kusitawi kwako itakuwa ni ndoto.
Najua wote tuna kucha na nywele. Siku moja nikiwa saloon(chegani). Nikamwambia kinyozi kuwa nataka anitengeneze vizuuri, yaani aninyoe nywele zote ziwe za "size" moja tena ndogo kabisa, Naye akafanya hivyo. Baada ya kutoka hapo kila mtu akaniambia kuwa nimependeza sana, Nikasema ahsante.
Lakini kadri siku zilivyoendelea kwenda ndivyo zile nywele ziliendelea kukua na baada ya wiki tatu tu. Daaaah! zikawa kubwa. Binafsi sikutambua zimekua lini na sangapi.
Vivyo hivyo kwa kucha tena. Kila nikizikata lakini baada ya muda tu naziona tena zimeshakuwa kubwa. kila nikizikata. Zinaota.
Ndipo nilipojifunza jambo moja kubwa sana. Hata kama tunakatishwa tamaa kwa kiasi gani, Pale ambapo tu unapojitambua kuwa una kila haja ya kuendelea mbele, Hakika utasitawi tena. Na utafanyika baraka kwa wale wanaokukatisha tamaa.
Yule kinyozi alijitahidi kuninyoa vizuri sana, na nikamlipa. Lengo lake ni kuzikatisha tamaa nywele zangu ili zisiwepo. Lakini baada ya mwezi nikarudi tena pale akaninyoa tena na nikamlipa tena.
Mpendwa,
Pale unapokata tamaa kumbuka kuwa kuna watu wanaathirika. Kuna watu wanaikosa Huduma yako. Wewe hapo ulipo ni fursa tosha.
Ukijitambua tu kuwa wewe ni fursa hakika hutakata tamaa. Wala hutakubali kukatishwa tamaa
Marafiki zako kila siku wanaoa na kuolewa lakini wewe bado. Wao wana watoto lakini wewe bado. Unabaki ukisononeka na kuona kama Mungu hakuoni kabisa. Tena kwa wale ambao wako makanisani wanaamua kuacha wokovu kabisa. Kisa tu wenzao wameolewa na kuoa. Kwanini unakata tamaa mapema hivyo??
Kumbuka madhara ya kukata tamaa hujikuta unatenda dhambi. Sara alipoahidiwa mtoto akasubiri kwa muda mrefu bila mafanikio akajikata akitenda dhambi ya kumshawishi mumewe Ibrahimu azae na mfanyakazi wake Hajiri.
Usikatshwe tamaa mpendwa nakutia moyo kuwa bado una nafasi ya kustawi tena.
Bado una nafasi ya kuinuliwa tena
Yesu akasema kuwa liko tumaini kwa mti uliokatwa ukachipua tena.
Naamini hata kwako lipo tumaini la kuchipua tena
Uchumi wako unaenda kuchipua tena,
Hayo mahusiano ambayo huyaelewielewi yanaenda kuchipua na kustawi tena
Familia yako inaenda kuchipua tena
Hata huduma yako inaenda kuchipua tena.
Yote haya yatatokea endapo tu hutakubali kukatishwa tamaa.
Mungu akuinue tena
Usisite kuwasiliana nasi kwa kuhitaji ushauri juu ya masuala mbalimbali ya kiroho na kimwli pia
Ndimi rafiki yako
Steven Mshiu
0655-882074

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MAKUNDI MAWILI YA WATU WANAOKUZUNGUKA.

FAHAMU MAKUNDI MAWILI YA WATU KATIKA MAISHA YAKO. Na Steven Mshiu . Maisha ya kila mwanadamu yamezungukwa na watu. Watu hawa waweza kat...