NGUVU YA MACHO.
Na Steven Mshiu,
Shalom watu wema wa Mungu. Naamini tumeianza wiki yetu vyema kabisa. Wiki iliyojaa ushindi mkubwa. Wiki itakayokuwa ya baraka sana kwako.
Leo nataka nikuletee makala hii fupi tu kuhusu nguvu ya macho.
Asilimia kubwa ya viumbe hai hususani wanyama vina macho. Mungu alipomuumba mwanadamu alimpa macho. Wakati wanyama wanapita mbele ya macho ya Adam, Alipowaangalia tu, akaanza kuwapa majina. Wewe utaitwa tembo, wewe utaitwa sungura. Bila shaka wewe utakuwa chura.
Kazi kubwa ya macho ni kupeleka taarifa kwenye ubongo, ili ubongo uweze kuanza kazi ya kuzichakata hizo taarifa ili kuleta majibu.
Kwa mfano,
Nimeona gari zuri au nyumba nzuri kwa kutumia macho. Sasa nataka nichore picha niliyoiona. Tayari macho yanapeleka ile picha ya gari au ile nyumba kwenye ubongo, Ubongo nao unaanza kazi ya kuchakata muonekano wa kitu nilichokiona halafu unakileta katika mchoro wa picha. Kwa hiyo inafanyika kazi ya kuhamisha ile nyumba niliyoiona, kutoka kwenye muonekano wake halisi halafu naileta kwenye mfumo wa picha.
Naweza kusema kazi kubwa ya macho ni kutransform kitu kutoka kwenye ule muonekano wake na kukipeleka kwenye ubongo ili kupata matokeo chanya au hasi, kutokana na ubongo utakavyoitafsiri hiyo picha.
Macho ni taa ya mwili. Kazi nyingine kubwa ya macho ni kuhakikisha kuwa mwili unakuwa salama kabisa. Siku moja nilikuwa natembea maeneo fulani, ghafla mbele yangu kulikuwa kuna nyoka. mguu haukuweza kumwona yule nyoka. Lakini macho ndiyo yaliyomwona yule nyoka, yakapeleka taarifa kwenye ubongo, ubongo nao nao ukapeleka taarifa kwenye miguu, kuwa ni wakati wa kukimbia.
Jana baada ya ibaada, nikawa nimekaa peke yangu huku nikitafakari mambo mengi kuhusu macho. Tafakari yangu ikaanzia kwenye Zaburi 119:37, "Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, unihuishe katika njia yako.
Anaeandika au anaesema maneno haya alishakutana na madhara ya matumizi mabaya ya macho. Wakati wanaume wameenda vitani yeye akabaki amelala gorofani kwake akamwona mwanamke anaoga, macho yake yakapeleka taarifa hasi kwenye ubongo wake na kumletea majibu kuwa ni vizuri akalala na huyo mwanamke, naye akafanya hivyo, Zaidi ya hapo bado akaongeza dhambi nyingine ya kuua kwa kukusudia. Huyu ni DAUDI 2 Samwel 11:1-5,
Nikaendelea mbele zaidi, nikakutana na mtu mwingine aliyeishi maisha ya utakatifu, ambaye alijitenga na dhambi kwa kiasi kikubwa sana, Biblia inamsifu kuwa alikuwa ni mtu mkamilifu sana, Hakupenda kumkosea Mungu Kwa namna yeyote ile. Hata aliposhawishiwa na marafiki zake na watu wake wa karibu amkufuru Mungu ili afe, yeye alikataa, Nikatafuta sana siri ya ushindi wake. Nikagundua kuwa yeye aliidhibiti nguvu ya macho yake. Huyu ni AYUBU.
Katika Ayubu 31:1, Anasema, "Nilifanya AGANO na MACHO yangu, Basi nawezaje kumwangalia msichana?"
Nikaendelea kujiuliza maswali mengi juu ya huyu Ayubu. Kwani kuna mvutano gani kati ya macho na msichana? Kwani hao wasichana wana tatizo gani? Anyway. Nikamkumbuka tena mtu anaeitwa YUSUPH na Mke wa Potifa. Yule mke wa Potifa alikuwa ni kikwazo kikubwa sana kwa Yusuph, Aliamini atakapovua nguo mbele ya Yusuph, basi hapo Yusuph hatakuwa na ujanja. Ni lazima angeingia kwenye kumi na nane zake kama wanavyosema vijana wa siku hizi. Lakini mtu huyu Yusufu naye alishafanya maagano na macho yake ili asimtende Mungu dhambi.
Nikasema labda hizo zilikuwa ni sheria za Agano la Kale.
Nilipokuja kwenye Agano Jipya Hapa ndipo niliishiwa nguvu kabisa. Maneno ya Yesu mwenyewe anahitimisha kwa kuonyesha nguvu ya macho. Kuwa macho yanaondoa kitu kutoka mfano wa picha na kukileta kwenye uhalisia.
Katika Mathayo 5:27-28, anasema, "Mmesikia imeandikwa usizini, Lakini mimi nawaambia kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamaniamekwisha kuzini naye moyoni mwake" Hapa nikafunga Biblia yangu nikasema Ee Mungu naomba nifanye Agano na macho yangu ili nisitazame visivyofaa, ili niweze kuwa hai na kubaki kwenye njia yako.
Haya macho yetu haya yatatusababisha tuikose mbingu hivi hivi, Siku moja nilishika simu ya kijana mmoja simu imejaa video zisizo na maadili ya mkristo, video za utupu, nikamuuliza ukishaangalia hizi video nini huwa kinafuata? Alikosa cha kunijibu nikamwambia unahitaji kuokoka upya.
Macho yetu huzalisha nguvu ya tamaa. Shetani alipojaribu kumpima Yesu kwa kutumia tamaa ya macho alimpandisha juu ya mlima mrefu na kumwonyesha milki zooote za dunia akidai kuwa atampa Yesu milki zote hizo endapo tu Yesu atamsujudia. Sio kwamba Yesu hakuziona hizo milki zote na uzuri wote. Yesu alikwisha fanya Agano na macho yake kuwa asitazame vitu vitakavyomtoa kwenye lile kusudi lake.
Watu wengi wamepoteza MAKUSUDI yao, kutokana na tamaa ya macho. Wengi wameshindwa kuizuia/control nguvu inayozalishwa na macho. Unaona mali nzuri ya mtu, badala ya kufanya kazi kwa bidii, na kuusumbua ubongo wako, unaruhusu taarifa kutoka kwa macho yako ambayo inaenda kuchakatwa kwenye ubongo wako ikuletee majibu ya kuiba hiyo mali. This is dangerous.
Ninapomalizia nitoe mtazamo wangu mimi kama mimi. Wahenga walisema kuwa macho hayana pazia. Viko vitu vingi tunaviona kwa macho yetu. Jambo la msingi ni kuyazuia au kuizuia taarifa ambayo macho yanaipeleka kwenye ubongo wako. Ukiona unatazama kitu halafu kikawa kinakuelekeza kuchukua maamuzi yasiyo mazuri chukua tahadhari kubwa. Yusufu alimkimbia mke wa Potifa. Akawa salama na akalitunza kusudi lake. Daudi yeye aliamua kuchukua hatua ya kulala na mke wa Uria.
Yesu yeye aliziona milki zote za dunia lakini akamjibu shetani hivi, "Nenda zako shetani. Imeandikwa msujudie Bwana Mungu wako umwabudu yeye peke yake"
Baada ya Yesu kumshinda shetani kwa kuizuia nguvu ya tamaa inayozalishwa na macho Biblia inaniambia kuwa shetani alimwacha na malaika wakaja kumtumikia Yesu.
Tunahitaji kuishi kwenye lengo. Ni lazima tupambane na hali zote zinazotutoa kwenye lengo. Sijui kwanini Biblia inapiga sana vita dhambi ya uzinzi. 2 petro 2:12.
Mungu anisaidie niidhibiti nguvu inayozalishwa na macho yangu
Steven Mshiu.
0655 882074
0768 882074
smshiu42@gmail.com
Na Steven Mshiu,
Shalom watu wema wa Mungu. Naamini tumeianza wiki yetu vyema kabisa. Wiki iliyojaa ushindi mkubwa. Wiki itakayokuwa ya baraka sana kwako.
Leo nataka nikuletee makala hii fupi tu kuhusu nguvu ya macho.
Asilimia kubwa ya viumbe hai hususani wanyama vina macho. Mungu alipomuumba mwanadamu alimpa macho. Wakati wanyama wanapita mbele ya macho ya Adam, Alipowaangalia tu, akaanza kuwapa majina. Wewe utaitwa tembo, wewe utaitwa sungura. Bila shaka wewe utakuwa chura.
Kazi kubwa ya macho ni kupeleka taarifa kwenye ubongo, ili ubongo uweze kuanza kazi ya kuzichakata hizo taarifa ili kuleta majibu.
Kwa mfano,
Nimeona gari zuri au nyumba nzuri kwa kutumia macho. Sasa nataka nichore picha niliyoiona. Tayari macho yanapeleka ile picha ya gari au ile nyumba kwenye ubongo, Ubongo nao unaanza kazi ya kuchakata muonekano wa kitu nilichokiona halafu unakileta katika mchoro wa picha. Kwa hiyo inafanyika kazi ya kuhamisha ile nyumba niliyoiona, kutoka kwenye muonekano wake halisi halafu naileta kwenye mfumo wa picha.
Naweza kusema kazi kubwa ya macho ni kutransform kitu kutoka kwenye ule muonekano wake na kukipeleka kwenye ubongo ili kupata matokeo chanya au hasi, kutokana na ubongo utakavyoitafsiri hiyo picha.
Macho ni taa ya mwili. Kazi nyingine kubwa ya macho ni kuhakikisha kuwa mwili unakuwa salama kabisa. Siku moja nilikuwa natembea maeneo fulani, ghafla mbele yangu kulikuwa kuna nyoka. mguu haukuweza kumwona yule nyoka. Lakini macho ndiyo yaliyomwona yule nyoka, yakapeleka taarifa kwenye ubongo, ubongo nao nao ukapeleka taarifa kwenye miguu, kuwa ni wakati wa kukimbia.
Jana baada ya ibaada, nikawa nimekaa peke yangu huku nikitafakari mambo mengi kuhusu macho. Tafakari yangu ikaanzia kwenye Zaburi 119:37, "Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, unihuishe katika njia yako.
Anaeandika au anaesema maneno haya alishakutana na madhara ya matumizi mabaya ya macho. Wakati wanaume wameenda vitani yeye akabaki amelala gorofani kwake akamwona mwanamke anaoga, macho yake yakapeleka taarifa hasi kwenye ubongo wake na kumletea majibu kuwa ni vizuri akalala na huyo mwanamke, naye akafanya hivyo, Zaidi ya hapo bado akaongeza dhambi nyingine ya kuua kwa kukusudia. Huyu ni DAUDI 2 Samwel 11:1-5,
Nikaendelea mbele zaidi, nikakutana na mtu mwingine aliyeishi maisha ya utakatifu, ambaye alijitenga na dhambi kwa kiasi kikubwa sana, Biblia inamsifu kuwa alikuwa ni mtu mkamilifu sana, Hakupenda kumkosea Mungu Kwa namna yeyote ile. Hata aliposhawishiwa na marafiki zake na watu wake wa karibu amkufuru Mungu ili afe, yeye alikataa, Nikatafuta sana siri ya ushindi wake. Nikagundua kuwa yeye aliidhibiti nguvu ya macho yake. Huyu ni AYUBU.
Katika Ayubu 31:1, Anasema, "Nilifanya AGANO na MACHO yangu, Basi nawezaje kumwangalia msichana?"
Nikaendelea kujiuliza maswali mengi juu ya huyu Ayubu. Kwani kuna mvutano gani kati ya macho na msichana? Kwani hao wasichana wana tatizo gani? Anyway. Nikamkumbuka tena mtu anaeitwa YUSUPH na Mke wa Potifa. Yule mke wa Potifa alikuwa ni kikwazo kikubwa sana kwa Yusuph, Aliamini atakapovua nguo mbele ya Yusuph, basi hapo Yusuph hatakuwa na ujanja. Ni lazima angeingia kwenye kumi na nane zake kama wanavyosema vijana wa siku hizi. Lakini mtu huyu Yusufu naye alishafanya maagano na macho yake ili asimtende Mungu dhambi.
Nikasema labda hizo zilikuwa ni sheria za Agano la Kale.
Nilipokuja kwenye Agano Jipya Hapa ndipo niliishiwa nguvu kabisa. Maneno ya Yesu mwenyewe anahitimisha kwa kuonyesha nguvu ya macho. Kuwa macho yanaondoa kitu kutoka mfano wa picha na kukileta kwenye uhalisia.
Katika Mathayo 5:27-28, anasema, "Mmesikia imeandikwa usizini, Lakini mimi nawaambia kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamaniamekwisha kuzini naye moyoni mwake" Hapa nikafunga Biblia yangu nikasema Ee Mungu naomba nifanye Agano na macho yangu ili nisitazame visivyofaa, ili niweze kuwa hai na kubaki kwenye njia yako.
Haya macho yetu haya yatatusababisha tuikose mbingu hivi hivi, Siku moja nilishika simu ya kijana mmoja simu imejaa video zisizo na maadili ya mkristo, video za utupu, nikamuuliza ukishaangalia hizi video nini huwa kinafuata? Alikosa cha kunijibu nikamwambia unahitaji kuokoka upya.
Macho yetu huzalisha nguvu ya tamaa. Shetani alipojaribu kumpima Yesu kwa kutumia tamaa ya macho alimpandisha juu ya mlima mrefu na kumwonyesha milki zooote za dunia akidai kuwa atampa Yesu milki zote hizo endapo tu Yesu atamsujudia. Sio kwamba Yesu hakuziona hizo milki zote na uzuri wote. Yesu alikwisha fanya Agano na macho yake kuwa asitazame vitu vitakavyomtoa kwenye lile kusudi lake.
Watu wengi wamepoteza MAKUSUDI yao, kutokana na tamaa ya macho. Wengi wameshindwa kuizuia/control nguvu inayozalishwa na macho. Unaona mali nzuri ya mtu, badala ya kufanya kazi kwa bidii, na kuusumbua ubongo wako, unaruhusu taarifa kutoka kwa macho yako ambayo inaenda kuchakatwa kwenye ubongo wako ikuletee majibu ya kuiba hiyo mali. This is dangerous.
Ninapomalizia nitoe mtazamo wangu mimi kama mimi. Wahenga walisema kuwa macho hayana pazia. Viko vitu vingi tunaviona kwa macho yetu. Jambo la msingi ni kuyazuia au kuizuia taarifa ambayo macho yanaipeleka kwenye ubongo wako. Ukiona unatazama kitu halafu kikawa kinakuelekeza kuchukua maamuzi yasiyo mazuri chukua tahadhari kubwa. Yusufu alimkimbia mke wa Potifa. Akawa salama na akalitunza kusudi lake. Daudi yeye aliamua kuchukua hatua ya kulala na mke wa Uria.
Yesu yeye aliziona milki zote za dunia lakini akamjibu shetani hivi, "Nenda zako shetani. Imeandikwa msujudie Bwana Mungu wako umwabudu yeye peke yake"
Baada ya Yesu kumshinda shetani kwa kuizuia nguvu ya tamaa inayozalishwa na macho Biblia inaniambia kuwa shetani alimwacha na malaika wakaja kumtumikia Yesu.
Tunahitaji kuishi kwenye lengo. Ni lazima tupambane na hali zote zinazotutoa kwenye lengo. Sijui kwanini Biblia inapiga sana vita dhambi ya uzinzi. 2 petro 2:12.
Mungu anisaidie niidhibiti nguvu inayozalishwa na macho yangu
Steven Mshiu.
0655 882074
0768 882074
smshiu42@gmail.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni