SIKU UWEPO WA MUNGU UKIONDOKA.
Na Steven Mshiu.
Aliomba mvua isinyeshe kwa muda wa miaka mitatu na nusu, nayo haikunyesha, MAANA UWEPO WA MUNGU ULIKUWA JUU YAKE.
Alishusha moto kutoka mbinguni ukaiteketeza ile sadaka.
Yule mwanamke wa Sarepta alibarikiwa kupita maelezo kwa neno lake.
Maana Uwepo wa Mungu ulikuwa juu yake.
Hata yule mtoto wa yule mjane aliyekuwa amekufa aliweza kufufuka kupitia yeye.
Aliweza kumthibitisha Mungu wake mbele ya wale manabii 450 wa Baali.
Na kwakuwa wale manabii wa Baali walishindwa kumthibitisha mungu wao aliweza kuwaua woote. Mtu mmoja akawaua watu 450 kwa ajili ya Mungu wake.
Lakini mtu huyu huyu aliyefanya mambo makubwa tena ya kuushangaza ulimwengu, alitishwa na mwanamke tu aliyeitwa Yezebeli, Akakimbia na kuketi chini ya mti huku akijiombea afe. Kwanini, Vitisho vya Yezebeli vilimfanya apoteze ule uwepo wa Mungu maishani mwake.
Huyu ndiye ELIYA aliyenyakuliwa kwa gari la moto. 1 Falme 16-19.
Alizaliwa kama mnadhiri wa Mungu.
Siku moja akiwa anaenda Timna alikutana na simba akamkamata na kumuua.
Alipotakiwa kulipa kile alichowaahidi wale watu juu ya kile kitendawili, aliweza kuwakamata wanaume 30 akawanyang'anya yale mavazi.
Walipomuudhi kwa kumchukua yule mchumba wake alikamata mbweha 300 akawafunga mikia wawili wawilihalafu akachoma ngano ya wafilisti.
walipojua kuwa yupo mjini wakapanga njama za kumkamata. Aling'oa lango(geti) kuu la mji halafu akalipeleka juu ya mlima. Huyu ni mtu mmoja tuu.
Akafika tena mji mmoja wakamkamata na kumfunga Roho wa Bwana akaja kwa nguvu juu yake akawaua watu 1000 kwa taya la punda.
Uwepo wa Mungu ulikuwa juu yake.
Mtu huyu huyu ndiye aliyekubali kulazwa kwnye mapaja ya Delila na akanyolewa nywele. Uwepo wa Mungu ukamtoka.
Hatimaye anakamatwa anatobolewa macho na kutupwa gerezani kisha anapewa kazi ya kusaga ngano.
Jina lake ni Samson. Amuzi 13-16.
Alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi wa Yesu.
Alitembea juu ya maji kwa Neno la Yesu. Akamkata sikio yule askari walipokuja kumkamata Yesu. Aliapa ataambatana na Yesu hadi kifo.
Lakini anakuja kutishiwa na kijakazi tu hatimaye akamkana Yesu
Huyu jina lake ni Petro.
Mpendwa,
Hakuna kitu cha maana kama kuutunza uwepo wa Mungu maishani mwako. Kamwe yeye hatakuacha. Ijapo tunaanguka ila tuna kila sababu ya kuuhitaji uwepo wa Mungu juu ya maisha yetu. Daudi alikuwa mkosaji mara nyingi sana, lakini aliutambua umuhimu wa uwepo wa Mungu juu ya maisha yake.
Nakukumbusha kuwa shetani hafurahii wewe kuwa chini ya uwepo wa Mungu. Anasubiri tu ufanye kosa dogo tu aanze kukunyanyasa. Anasubiri uanguke kwenye dhambi aanze kukutesa.
Anakusubiri akutoboe macho kama Samson.
Anasubiri uwepo wa Mungu ukuondokee aanze kukutia hofu ya kujiua.
Anatumia mbinu nyingi sana kuhakikisha anakunyanyasa.
Lakini nakutia moyo kuwa, bado una nafasi ya kuuhitaji uwepo wa Mungu juu ya maisha yako kwa nafasi nyingine.
Eliya alipokuwa chini ya mretemu Mungu alimtia moyo kuwa Safari bado ni mbichi.
Samson alikuja kuwaua watu wengi zaidi ya wale aliokwisha kuwaua hapo mwanzo,n.k
Nikutahadharishe jambo moja. Usifikiri kuutunza uwepo wa Mungu ni kazi rahisi. Kuna gharama za kulipa. Gharama za kuutunza uwepo wa Mungu ni kuishi maisha ya Utakatifu. Maisha ya kujikana. Maisha ya kujitenga dhambi. Vinginevyo utakugarimu uhai wako kama Samson.
Steven Mshiu.
Na Steven Mshiu.
Aliomba mvua isinyeshe kwa muda wa miaka mitatu na nusu, nayo haikunyesha, MAANA UWEPO WA MUNGU ULIKUWA JUU YAKE.
Alishusha moto kutoka mbinguni ukaiteketeza ile sadaka.
Yule mwanamke wa Sarepta alibarikiwa kupita maelezo kwa neno lake.
Maana Uwepo wa Mungu ulikuwa juu yake.
Hata yule mtoto wa yule mjane aliyekuwa amekufa aliweza kufufuka kupitia yeye.
Aliweza kumthibitisha Mungu wake mbele ya wale manabii 450 wa Baali.
Na kwakuwa wale manabii wa Baali walishindwa kumthibitisha mungu wao aliweza kuwaua woote. Mtu mmoja akawaua watu 450 kwa ajili ya Mungu wake.
Lakini mtu huyu huyu aliyefanya mambo makubwa tena ya kuushangaza ulimwengu, alitishwa na mwanamke tu aliyeitwa Yezebeli, Akakimbia na kuketi chini ya mti huku akijiombea afe. Kwanini, Vitisho vya Yezebeli vilimfanya apoteze ule uwepo wa Mungu maishani mwake.
Huyu ndiye ELIYA aliyenyakuliwa kwa gari la moto. 1 Falme 16-19.
Alizaliwa kama mnadhiri wa Mungu.
Siku moja akiwa anaenda Timna alikutana na simba akamkamata na kumuua.
Alipotakiwa kulipa kile alichowaahidi wale watu juu ya kile kitendawili, aliweza kuwakamata wanaume 30 akawanyang'anya yale mavazi.
Walipomuudhi kwa kumchukua yule mchumba wake alikamata mbweha 300 akawafunga mikia wawili wawilihalafu akachoma ngano ya wafilisti.
walipojua kuwa yupo mjini wakapanga njama za kumkamata. Aling'oa lango(geti) kuu la mji halafu akalipeleka juu ya mlima. Huyu ni mtu mmoja tuu.
Akafika tena mji mmoja wakamkamata na kumfunga Roho wa Bwana akaja kwa nguvu juu yake akawaua watu 1000 kwa taya la punda.
Uwepo wa Mungu ulikuwa juu yake.
Mtu huyu huyu ndiye aliyekubali kulazwa kwnye mapaja ya Delila na akanyolewa nywele. Uwepo wa Mungu ukamtoka.
Hatimaye anakamatwa anatobolewa macho na kutupwa gerezani kisha anapewa kazi ya kusaga ngano.
Jina lake ni Samson. Amuzi 13-16.
Alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi wa Yesu.
Alitembea juu ya maji kwa Neno la Yesu. Akamkata sikio yule askari walipokuja kumkamata Yesu. Aliapa ataambatana na Yesu hadi kifo.
Lakini anakuja kutishiwa na kijakazi tu hatimaye akamkana Yesu
Huyu jina lake ni Petro.
Mpendwa,
Hakuna kitu cha maana kama kuutunza uwepo wa Mungu maishani mwako. Kamwe yeye hatakuacha. Ijapo tunaanguka ila tuna kila sababu ya kuuhitaji uwepo wa Mungu juu ya maisha yetu. Daudi alikuwa mkosaji mara nyingi sana, lakini aliutambua umuhimu wa uwepo wa Mungu juu ya maisha yake.
Nakukumbusha kuwa shetani hafurahii wewe kuwa chini ya uwepo wa Mungu. Anasubiri tu ufanye kosa dogo tu aanze kukunyanyasa. Anasubiri uanguke kwenye dhambi aanze kukutesa.
Anakusubiri akutoboe macho kama Samson.
Anasubiri uwepo wa Mungu ukuondokee aanze kukutia hofu ya kujiua.
Anatumia mbinu nyingi sana kuhakikisha anakunyanyasa.
Lakini nakutia moyo kuwa, bado una nafasi ya kuuhitaji uwepo wa Mungu juu ya maisha yako kwa nafasi nyingine.
Eliya alipokuwa chini ya mretemu Mungu alimtia moyo kuwa Safari bado ni mbichi.
Samson alikuja kuwaua watu wengi zaidi ya wale aliokwisha kuwaua hapo mwanzo,n.k
Nikutahadharishe jambo moja. Usifikiri kuutunza uwepo wa Mungu ni kazi rahisi. Kuna gharama za kulipa. Gharama za kuutunza uwepo wa Mungu ni kuishi maisha ya Utakatifu. Maisha ya kujikana. Maisha ya kujitenga dhambi. Vinginevyo utakugarimu uhai wako kama Samson.
Steven Mshiu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni