Na Steven Mshiu
Mwaka jana nikiwa na rafiki yangu Elias Kisingi, tulipata muda mzuri wa kujifunza juu ya kitabu cha Ayubu sura hadi sura.
Tulitumia zaidi ya miezi mitatu tukijifunza juu ya kitabu hiki kuanzia maisha ya Ayubu. huduma yake, njia zake pamoja na mambo mengi sana.
Maisha ya Ayubu yalikuwa ni mfano tosha na kielelezo kwa wanadamu wote
waliopo juu ya uso wa dunia. Biblia inamsifu kuwa alikuwa ni mtu
mkamilifu wala hila haikuonekana ndani yake.
Maisha yake ya kiroho sichelei kusema kuwa yalikuwa ni ya viwango vya hali ya juu. Alitambua maana ya kumtolea mungu, Mara nyingi alitoa sadaka za kuomba rehema kwa Mungu juu ya familia yake.
Wakati fulani Mungu aliruhusu shetani amjaribu Ayubu. Ayubu huyu ambaye hakuwa mtenda dhambi akaanza kupitia katika vipindi vigumu sana katika maisha yake. Mali zake zikaisha, watoto wakafariki. Hali yake ya kiuchumi ikawa mbaya sana. Kumbuka Biblia inaposema kuwa alikuwa ni tajiri, ni tajiri kweli kweli. Licha ya kuwa tajiri Ayubu alimcha Mungu.
Kama unavyofahamu kuwa mtu anapokuwa tajiri huwa na marafiki wengi sana. Jambo la muhimu la kufahamu je siku ukiishiwa hao marafiki watakuwa na wewe.
Hali ilipozidi kuwa mbaya kwa Ayubu, walewale marafiki zake waliokuwa wakila pamoja, wakinywa pamoja na kufanya mambo mengi kwa pamoja walimkimbia, Wakadiriki kusema kuwa Ayubu ametenda dhambi. Lakini haikuwa hivyo.
Hata mtu wa karibu sana wa Ayubu ambaye walilala kitanda kimoja alidiriki kufika hatua ya kumwambia Ayubu amkufuru Mungu ili afe.
Kitu ambacho nilitaka kukukumbusha ni kwamba ni vyema ukasimama wewe kama wewe mwenyewe pale unapopatwa au kukumbwa na chochote. Mara nyingi wale watu wa karibu wanaweza wakakuacha, mke wako anaweza akakuacha, familia yako ikakuacha, hata mpenzi wako akakuacha. Watu hawa wanaweza wakawa na dhamira nzuri za kukusaidia lakini dhamira zao zikawa ni anguko kwako, Kama Ayubu angefuata ushauri wa mke wake nahisi angekuwa ni mtu wa ajabu sana.
Kila mtu anapokuwa kinyume na wewe, jitahidi kusimamia kile unachokiamini. Ayubu hakufuata ushauri wa akina Elifasi, Elihu, Bilidadi wala mke wake. Biblia inaniambia kuwa mwisho wa Ayubu ulikuwa mkubwa kuliko ule mwanzo wake. Alibarikiwa zaidi kuliko ilivyokuwa mwanzo.
Kwanini?
Ayubu alisimama peke yake ingawa kila mtu alikuwa kinyume na yeye.
Mungu amekusudia kuufanya mwisho wako kuwa bora zaidi ya mwanzo wako. Lile wazo la biashara ulilo nalo kuna watu umewaambia, lakini mawazo yao ni kama yale ya mke wa Ayubu, Wengine wanakuambia huwezi kufanikiwa kupitia wazo hilo. Ni wakati wako wa kusimama peke yako.
Mwisho mzuri unaandaliwa na mwanzo mzuri. Mwanzo mzuri ni yale mawazo ya kwanza kabisa yanayotokea kwenye akili yako. Unatamani kuwa mtumishi mkubwa wa Mungu lakini kuna watu wana roho ya Herode au ya Farao ya kutaka kumuua mtoto, Ni wakati wako kusimama peke yako.
Steven Mshiu
Maisha yake ya kiroho sichelei kusema kuwa yalikuwa ni ya viwango vya hali ya juu. Alitambua maana ya kumtolea mungu, Mara nyingi alitoa sadaka za kuomba rehema kwa Mungu juu ya familia yake.
Wakati fulani Mungu aliruhusu shetani amjaribu Ayubu. Ayubu huyu ambaye hakuwa mtenda dhambi akaanza kupitia katika vipindi vigumu sana katika maisha yake. Mali zake zikaisha, watoto wakafariki. Hali yake ya kiuchumi ikawa mbaya sana. Kumbuka Biblia inaposema kuwa alikuwa ni tajiri, ni tajiri kweli kweli. Licha ya kuwa tajiri Ayubu alimcha Mungu.
Kama unavyofahamu kuwa mtu anapokuwa tajiri huwa na marafiki wengi sana. Jambo la muhimu la kufahamu je siku ukiishiwa hao marafiki watakuwa na wewe.
Hali ilipozidi kuwa mbaya kwa Ayubu, walewale marafiki zake waliokuwa wakila pamoja, wakinywa pamoja na kufanya mambo mengi kwa pamoja walimkimbia, Wakadiriki kusema kuwa Ayubu ametenda dhambi. Lakini haikuwa hivyo.
Hata mtu wa karibu sana wa Ayubu ambaye walilala kitanda kimoja alidiriki kufika hatua ya kumwambia Ayubu amkufuru Mungu ili afe.
Kitu ambacho nilitaka kukukumbusha ni kwamba ni vyema ukasimama wewe kama wewe mwenyewe pale unapopatwa au kukumbwa na chochote. Mara nyingi wale watu wa karibu wanaweza wakakuacha, mke wako anaweza akakuacha, familia yako ikakuacha, hata mpenzi wako akakuacha. Watu hawa wanaweza wakawa na dhamira nzuri za kukusaidia lakini dhamira zao zikawa ni anguko kwako, Kama Ayubu angefuata ushauri wa mke wake nahisi angekuwa ni mtu wa ajabu sana.
Kila mtu anapokuwa kinyume na wewe, jitahidi kusimamia kile unachokiamini. Ayubu hakufuata ushauri wa akina Elifasi, Elihu, Bilidadi wala mke wake. Biblia inaniambia kuwa mwisho wa Ayubu ulikuwa mkubwa kuliko ule mwanzo wake. Alibarikiwa zaidi kuliko ilivyokuwa mwanzo.
Kwanini?
Ayubu alisimama peke yake ingawa kila mtu alikuwa kinyume na yeye.
Mungu amekusudia kuufanya mwisho wako kuwa bora zaidi ya mwanzo wako. Lile wazo la biashara ulilo nalo kuna watu umewaambia, lakini mawazo yao ni kama yale ya mke wa Ayubu, Wengine wanakuambia huwezi kufanikiwa kupitia wazo hilo. Ni wakati wako wa kusimama peke yako.
Mwisho mzuri unaandaliwa na mwanzo mzuri. Mwanzo mzuri ni yale mawazo ya kwanza kabisa yanayotokea kwenye akili yako. Unatamani kuwa mtumishi mkubwa wa Mungu lakini kuna watu wana roho ya Herode au ya Farao ya kutaka kumuua mtoto, Ni wakati wako kusimama peke yako.
Steven Mshiu
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni