TAFUTA KUWA NA UTOFAUTI
Habarini za asubuhi wapendwa. Ni matumaini yangu kuwa mmeamka mkiwa na nguvu na afya tele ambayo tumepewa bure na Muumba wetu.
Nikupongeze wewe ambaye tayari umeshayaanza majukumu yako ya kila siku ya kujitafutia riziki ili mkono uweze kwenda kinywani. Biblia inatuagiza kufanya kazi. Hivyo ni vyema ukazidi kuweka juhudi kubwa juu ya kile unachokifanya.
Kila siku tunapitia mambo au changamoto ambazo tunajifunza kutokana nazo.
Moja ya changamoto ambayo tunakutana nayo ni ile hali ya kushindwa kujitofautisha.
Kuna mtu unaweza kumkuta mahali fulani na ameridhika na sehemu ile alipo lakini kwa hadhi na heshima yake asingestahili kuwepo sehemu hiyo. Kwa mfano, huku kwetu uchagani kuna vilabu vya pombe ya kienyeji huwa wanaiita mbege, Itashangaza sana kumkuta mchungaji au mtumishi wa Mungu ameketi kilabuni pamoja na wanywaji wa pombe hiyo bila sababu maalum. Mtu huyo atakuwa ameshindwa kujitofautisha.
Au umkute kiongozi mkubwa wa serikali amekaa kijiweni na watu wasiokuwa na kazi wakipiga hadithi tu bila mantiki yoyote. Kiongozi huyo atakuwa na walakini mkubwa sana.
Kipindi cha huduma ya Yesu, mara nyingi alijitofautisha sana na Wayahudi kuanzia usemi, namna ya kuishi n.k. Sababu za kujitofautisha ni ili ile kazi yake au huduma yake aliyokuwa akiifanya iweze kukubalika.
Utofauti unakufanya uwe mtu wa tofauti. Mtu wa tofauti ni lazima afanye mambo tofauti kabisa na yale wanayoyafanya watu walioshindwa kujitofautisha. Unapofanya kitu cha tofauti mara nyingi kitu hicho hudumu kwa muda kwa muda mrefu lakini endapo utafanya kitu au jambo lolote kwa mazoea jambo hilo haliwezi kudumu kwa muda mrefu.
Ngoja nikupe ushuhuda huu mfupi, Siku tatu zilizopita nikiwa nimetoka kazini kwangu, Mara nyingi huwa natumia usafiri wa daladala. Nikapanda daladala moja hivi kutokana ile hali ya uchovu wa siku nzima nikawa nimetulia tu kwenye moja seat ya katikati ya daladala hiyo, mbele yangu walikaa watu wanne na nyuma yangu walikaa watu wanne pia.
Tukaanza safari, Nilipoangalia wale waliokuwa wamekaa mbele yangu walikuwa busy sana na smartphone zao, kuna mbao walikuwa wakiangalia nyimbo kwenye Youtube, wengine walikuwa wakichat faceook na whatsapp, vivyohivyo hata wale wa nyuma yangu nao walikuwa very busy kuchat, na kuangalia video/nyimbo kwenye youtube.
Nikawaangalia tena wale abiria waliokaa pembeni yangu nao pia walikuwa busy kuangalia mitindo ya nguo na nywele kwenye simu zao. Nikawaza sana. Hivi na mimi nitoe simu yangu nianze kuperuzi facebook na Whatsapp?
Nikasikia sauti ikiniambia tafuta kuwa tofauti na hawa wote, nikawaza sana nitawezaje kuwa tofauti nao? Kwa bahati nzuri nilikuwa nimebeba Biblia yangu kwenye bahasha ya A4, nikaitoa bila woga wala wasiwasi na nikaanza kujisomea zangu Biblia.
Nami nikawa very busy nikiperuzi baadhi ya mistari kwenye Biblia yangu. Jambo la kushangaza na la ajabu wale waliokuwa very busy wakichati walibadilisha topic na kuanza kusema huyu kaka atakuwa ameokoka. Nami bila kusita nikawajibu Bila shaka. Hatimaye safari yetu ikazidi kusonga mbele.
Wakaanza kuniuliza maswali kuhusu Biblia, nami nikawajibu. Hivyo nikafanikiwa kuwabadilisha kile walichokuwa wakikifanya wakajiunga nami.
Nikajifunza jambo lingine kuwa watu wako tayari kukufuata kwenye kile unachokifanya endapo utaonyesha utofauti. Kijana niliyeokoka niwe tofauti na wale ambao hawajaokoka. Wao wakivalia suruali chini ya makalio basi mimi nivalie kiunoni vizuri tena nimechomekea ikibidi na tai nifunge. Kwanini? Natafuta utofauti.
Binti uliyeokoka wakati wenzako wamevalia nusu uchi, basi wewe waonyeshe utofauti kwa kuvalia mavazi yanayousitiri mwili wako. Wakati wao wanatafuta kuufanania ulimwengu wewe tafuta utofauti kwa kutaka kumfanania Kristo, kuanzia usemi wako, mwenendo wako, na hata maisha yako ya ujumla.
Heshima hufuata utofauti. Unaweza kujikuta unaitwa majina fulani fulani kwa sababu tu umeonyesha utofauti au umeshindwa kuonyesha utofauti, Kulikuwa na wana wa Sikewa wao walipokutana na mtu mwenye pepo wakaanza kumkemea kwa Jina la Yesu anaehubiriwa na Paulo, Pepo wakamjibu Paulo tunamfahamu, Na hata Yesu tunamfahamu. Je ninyi ni akina nani? Watu hawa walishindwa kutambua tofauti iliyopo kati yao na Paulo. Wakajikuta wakiaibika mbele ya pepo. Mdo 19:13-16
Epuka kufanya vitu kwa mazoea au namna wenzako wanavyofanya. Wewe umeumbwa kwa utofauti. Wewe ni tofauti na mimi, Na hata mimi ni tofauti kabisa na wewe. Mungu anampenda mtu anayefanya vitu vya tofauti. Lakini tofauti ninayizungumzia hapa ni ile inayojenga tu. Ukitafuta kufanya vitu vya utofauti wenye tofauti hasi imekula kwako.
Yuda Iskariote yeye alitafuta utofauti wake kwa kumsaliti Yesu, Kilichomkuta ni siri yake mwenyewe.
Nikutie moyo.
Yawezekana umekuwa ukifanya mambo kwa hali ya ukawaida tu, Leo una nafasi ya kuanza kufanya kwa hali ya tofauti kabisa. Usijali dunia itakuonaje. Au watu watakusemaje. Wewe fanya jambo la tofauti.
Jifunze kwa Elisha na Eliya. Kipindi Eliya anakaribia kunyakuliwa kwa magari ya moto, Elisha alidhamiria kumfuata hadi mwisho.
Licha ya kukatishwa na tamaa na miongoni mwa watu wa karibu naye tena manabii, yeye aliwajibu jibu moja tu, Ndio. Nafahamu atanyakuliwa ila niacheni. Elisha alitafuta kuwa tofauti na mawazo ya wale manabii. Mwishowe wale manabii walikuja kuwa chini ya Elisha.
Mungu amekusudia kukuweka sehemu fulani. Amekusudia kukubariki. Amekusudia kukufanyia muujiza mkubwa kwenye kazi yako, kwenye biashara yako, kwenye masomo yako, kwenye familia yako au popote pale utakapopita endapo utaamua kuonyesha utofauti tu.
Mungu akubariki sana kwa kuwa utatafuta kuwa wa tofauti.
Na Steven Mshiu
+255 655 882074
+255 768 882074
Habarini za asubuhi wapendwa. Ni matumaini yangu kuwa mmeamka mkiwa na nguvu na afya tele ambayo tumepewa bure na Muumba wetu.
Nikupongeze wewe ambaye tayari umeshayaanza majukumu yako ya kila siku ya kujitafutia riziki ili mkono uweze kwenda kinywani. Biblia inatuagiza kufanya kazi. Hivyo ni vyema ukazidi kuweka juhudi kubwa juu ya kile unachokifanya.
Kila siku tunapitia mambo au changamoto ambazo tunajifunza kutokana nazo.
Moja ya changamoto ambayo tunakutana nayo ni ile hali ya kushindwa kujitofautisha.
Kuna mtu unaweza kumkuta mahali fulani na ameridhika na sehemu ile alipo lakini kwa hadhi na heshima yake asingestahili kuwepo sehemu hiyo. Kwa mfano, huku kwetu uchagani kuna vilabu vya pombe ya kienyeji huwa wanaiita mbege, Itashangaza sana kumkuta mchungaji au mtumishi wa Mungu ameketi kilabuni pamoja na wanywaji wa pombe hiyo bila sababu maalum. Mtu huyo atakuwa ameshindwa kujitofautisha.
Au umkute kiongozi mkubwa wa serikali amekaa kijiweni na watu wasiokuwa na kazi wakipiga hadithi tu bila mantiki yoyote. Kiongozi huyo atakuwa na walakini mkubwa sana.
Kipindi cha huduma ya Yesu, mara nyingi alijitofautisha sana na Wayahudi kuanzia usemi, namna ya kuishi n.k. Sababu za kujitofautisha ni ili ile kazi yake au huduma yake aliyokuwa akiifanya iweze kukubalika.
Utofauti unakufanya uwe mtu wa tofauti. Mtu wa tofauti ni lazima afanye mambo tofauti kabisa na yale wanayoyafanya watu walioshindwa kujitofautisha. Unapofanya kitu cha tofauti mara nyingi kitu hicho hudumu kwa muda kwa muda mrefu lakini endapo utafanya kitu au jambo lolote kwa mazoea jambo hilo haliwezi kudumu kwa muda mrefu.
Ngoja nikupe ushuhuda huu mfupi, Siku tatu zilizopita nikiwa nimetoka kazini kwangu, Mara nyingi huwa natumia usafiri wa daladala. Nikapanda daladala moja hivi kutokana ile hali ya uchovu wa siku nzima nikawa nimetulia tu kwenye moja seat ya katikati ya daladala hiyo, mbele yangu walikaa watu wanne na nyuma yangu walikaa watu wanne pia.
Tukaanza safari, Nilipoangalia wale waliokuwa wamekaa mbele yangu walikuwa busy sana na smartphone zao, kuna mbao walikuwa wakiangalia nyimbo kwenye Youtube, wengine walikuwa wakichat faceook na whatsapp, vivyohivyo hata wale wa nyuma yangu nao walikuwa very busy kuchat, na kuangalia video/nyimbo kwenye youtube.
Nikawaangalia tena wale abiria waliokaa pembeni yangu nao pia walikuwa busy kuangalia mitindo ya nguo na nywele kwenye simu zao. Nikawaza sana. Hivi na mimi nitoe simu yangu nianze kuperuzi facebook na Whatsapp?
Nikasikia sauti ikiniambia tafuta kuwa tofauti na hawa wote, nikawaza sana nitawezaje kuwa tofauti nao? Kwa bahati nzuri nilikuwa nimebeba Biblia yangu kwenye bahasha ya A4, nikaitoa bila woga wala wasiwasi na nikaanza kujisomea zangu Biblia.
Nami nikawa very busy nikiperuzi baadhi ya mistari kwenye Biblia yangu. Jambo la kushangaza na la ajabu wale waliokuwa very busy wakichati walibadilisha topic na kuanza kusema huyu kaka atakuwa ameokoka. Nami bila kusita nikawajibu Bila shaka. Hatimaye safari yetu ikazidi kusonga mbele.
Wakaanza kuniuliza maswali kuhusu Biblia, nami nikawajibu. Hivyo nikafanikiwa kuwabadilisha kile walichokuwa wakikifanya wakajiunga nami.
Nikajifunza jambo lingine kuwa watu wako tayari kukufuata kwenye kile unachokifanya endapo utaonyesha utofauti. Kijana niliyeokoka niwe tofauti na wale ambao hawajaokoka. Wao wakivalia suruali chini ya makalio basi mimi nivalie kiunoni vizuri tena nimechomekea ikibidi na tai nifunge. Kwanini? Natafuta utofauti.
Binti uliyeokoka wakati wenzako wamevalia nusu uchi, basi wewe waonyeshe utofauti kwa kuvalia mavazi yanayousitiri mwili wako. Wakati wao wanatafuta kuufanania ulimwengu wewe tafuta utofauti kwa kutaka kumfanania Kristo, kuanzia usemi wako, mwenendo wako, na hata maisha yako ya ujumla.
Heshima hufuata utofauti. Unaweza kujikuta unaitwa majina fulani fulani kwa sababu tu umeonyesha utofauti au umeshindwa kuonyesha utofauti, Kulikuwa na wana wa Sikewa wao walipokutana na mtu mwenye pepo wakaanza kumkemea kwa Jina la Yesu anaehubiriwa na Paulo, Pepo wakamjibu Paulo tunamfahamu, Na hata Yesu tunamfahamu. Je ninyi ni akina nani? Watu hawa walishindwa kutambua tofauti iliyopo kati yao na Paulo. Wakajikuta wakiaibika mbele ya pepo. Mdo 19:13-16
Epuka kufanya vitu kwa mazoea au namna wenzako wanavyofanya. Wewe umeumbwa kwa utofauti. Wewe ni tofauti na mimi, Na hata mimi ni tofauti kabisa na wewe. Mungu anampenda mtu anayefanya vitu vya tofauti. Lakini tofauti ninayizungumzia hapa ni ile inayojenga tu. Ukitafuta kufanya vitu vya utofauti wenye tofauti hasi imekula kwako.
Yuda Iskariote yeye alitafuta utofauti wake kwa kumsaliti Yesu, Kilichomkuta ni siri yake mwenyewe.
Nikutie moyo.
Yawezekana umekuwa ukifanya mambo kwa hali ya ukawaida tu, Leo una nafasi ya kuanza kufanya kwa hali ya tofauti kabisa. Usijali dunia itakuonaje. Au watu watakusemaje. Wewe fanya jambo la tofauti.
Jifunze kwa Elisha na Eliya. Kipindi Eliya anakaribia kunyakuliwa kwa magari ya moto, Elisha alidhamiria kumfuata hadi mwisho.
Licha ya kukatishwa na tamaa na miongoni mwa watu wa karibu naye tena manabii, yeye aliwajibu jibu moja tu, Ndio. Nafahamu atanyakuliwa ila niacheni. Elisha alitafuta kuwa tofauti na mawazo ya wale manabii. Mwishowe wale manabii walikuja kuwa chini ya Elisha.
Mungu amekusudia kukuweka sehemu fulani. Amekusudia kukubariki. Amekusudia kukufanyia muujiza mkubwa kwenye kazi yako, kwenye biashara yako, kwenye masomo yako, kwenye familia yako au popote pale utakapopita endapo utaamua kuonyesha utofauti tu.
Mungu akubariki sana kwa kuwa utatafuta kuwa wa tofauti.
Na Steven Mshiu
+255 655 882074
+255 768 882074
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni