UKIRUDI NYUMA HATUA MOJA SONGA MBELE HATUA TANO.
Na Steven Mshiu.
Habarini za muda huu watu wa Mungu.
Naamini umeamka u bukheri wa afya.
Tumshukuru Mungu kwa pumzi aliyotujalia kila leo,
Mara nyingi tumekuwa tukikutana na mambo au changamoto ambazo huturudisha nyuma na kutufanya kujenga dhana ya kushindwa.
Leo nataka nikutie moyo kuwa endapo utarudi nyuma hatua moja bado una nafasi ya kusonga mbele hatua tano.
Jana nilikuwa nasafiri kutoka eneo fulani hadi eneo jingine. safari iliyochukua muda wa kama masaa mawili hivi. Kwa bahati nzuri nilikaa karibu kabisa na dereva. Muda mwingi niliutumia kumuangalia yule dereva jinsi anavyoendesha gari.
Ili gari iweze kwenda alikuwa akitumia "gia"
Ikabidi nitumie nguvu kubwa zaidi kuangalia kile "kirungu" au gia ni namna gani kinavyotumika.
Nilipoangalia kwa umakini sana pale juu ya kile kirungu niliona namba 1,2,3,4,5 na R.
Mwanzo wa safari yetu wakati tunaondoka pale stendi, Kile kirungu alikielekeza kwenye herufi R, nikaona gari ikirudi nyuma maana kuna gari nyingine iliyokuwa mbele yetu. Baada ya kurudi nyuma kidogo na palipopatikana upenyo wa ile gari yetu kupita, dereva alielekeza kile kirungu kwenye namba 1 hatimaye nikaona gari ikienda mbele.
Kadri tulivyoendelea mbele dereva alikuwa akihamisha kile kirungu kutoka namba hadi namba. Yaani alitoka 1 hadi 2 akaendelea 3,4 hadi 5. Sikumwona akitumia tena au akilekeza kile kirungu kwenye herufi R.
Hata wakati alipotaka kupakia barabarani sikumwona akirudisha kile kirungu kwenye herufi R, mara nyingi alikuwa akikiacha kikiwa katikati, na alipomaliza kupakia abiria alikielekeza kwenye namba 1 gari ikasonga mbele kwa mbele.
Baada ya kutumia muda mrefu saaana kumuangalia yule dereva, huku nikizalisha maswali mengi kichwani, nilishindwa kuvumilia ikabidi nimuulize yule dereva. Mbona huelekezi hicho kirungu kwenye hiyo herufi R? Mbona umekitumia mara moja tuu.
Ndipo akaniambia kuwa Hiyo herufi R ni gia ya kurudi nyuma, mara nyingi tunapoendesha gari gia hii huwa tunaitumia mara chache sana, haswa kwa biashara zetu hizi za kubeba abiria. Abiria wao wanaenda mbele, sasa tukiweka hii gia ya kurudi nyuma hawatafika na sisi hatutapata pesa, maana tutakuwa tunarudi nyuma tu, Wakati ananiambia maneno haya alikuwa akihama kutoka namba 3 hadi 4, huku gari ikizidi kuongeza mwendo tofauti na ule wa wakati ameweka namba1.
Nikamwambia ahsante kwa majibu yako. Lakini mbona ukihama kutoka namba 1 au 2 unapohamia 3 au 4 mwendo unaongezeka? Akaniambia siku zote unapoanza safari huwa ngumu sana au nzito lakini kadri unavyosonga mbele safari huwa nyepesi, hivyo ninavyobadili gia kutoka 1,2 kwenda 3 au 4 gari huwa nyepesi sana hivyo mwendo nao unaongezeka.
Kila alipozidi kubadili gia ndivyo ambavyo mwendo uliongezeka.
Nikamsikia "konda" akigonga bodi akiashiria kuwa ameona abiria anaetaka kuingia kwenye gari. Wakati huo dereva alikuwa kwenye gia namba 5, wakati anasimamisha gari alianza kurudi gia za nyuma yaani 4, 3, 2 hadi 1. Nilichoshangaa tena wakati anabadili gia hizi kurudi nyuma gari nayo ilikuwa ikipunguza mwendo.
Nilijifunza mambo mengi sana kuhusu mfumo huu unaotumiwa na gari hili.
Katika maisha yetu ni vyema tukajitengenezea mfumo kama wa gari. Unapoianza safari mara nyingi hurudi nyuma kuangalia mwanzo wako, Ni namna gani mbele yako kulikuwa na vikwazo vingi vinavyokuzuia wewe usisonge mbele, rudi nyuma mara moja tu, utengeneze mwanya wa wewe kusonga mbele. Yule dereva alirudi nyuma mara moja tu ili kukwepa ile gari iliyokuwa mbele yake.
Ni lazima ukubali kurudi nyuma mara moja tu, yule dereva angeng'ang'ania kuweka gia za mbele angeweza kusababisha ajali na safari yake ingekwama.
Unapoanza kusonga mbele, mara nyingi mwanzo huwa mzito. lakini kadri unavyozidi kubadili gia za kusonga mbele safari huwa nyepesi yale mazito uliyokuwa ukiyaona yanakuwa mepesi. Kadri unavyozidi kwenda mbele ndivyo ambavyo unazidi kutengeneza fursa nyingi zinazokuletea faida.
UKIRUDI NYUMA MARA MOJA SONGA MBELE MARA TANO ZAIDI
Usikubali kurudi nyuma mara nyingi. Ukiwa jeshini yule anayeonekana kurudi nyuma huwa anapigwa risasi. Kwenye daladala dereva akianza kuweka gia ya kurudi nyuma tu, hakuna abiria atakaepanda gari hiyo. Matokeo yake watakosa pesa.
Ukikubali au ukiruhusu kuwa mtu wa kurudi nyuma tu, jiandae kupigwa risasi, jiandae kukosa abiria, jiandae kukosa fursa.
Ukianza jambo jitahidi lisonge mbele na wala sio kurudi nyuma.
Insipired by Steven Mshiu.
+255 655 882074

Habarini za muda huu watu wa Mungu.
Naamini umeamka u bukheri wa afya.
Tumshukuru Mungu kwa pumzi aliyotujalia kila leo,
Mara nyingi tumekuwa tukikutana na mambo au changamoto ambazo huturudisha nyuma na kutufanya kujenga dhana ya kushindwa.
Leo nataka nikutie moyo kuwa endapo utarudi nyuma hatua moja bado una nafasi ya kusonga mbele hatua tano.
Jana nilikuwa nasafiri kutoka eneo fulani hadi eneo jingine. safari iliyochukua muda wa kama masaa mawili hivi. Kwa bahati nzuri nilikaa karibu kabisa na dereva. Muda mwingi niliutumia kumuangalia yule dereva jinsi anavyoendesha gari.
Ili gari iweze kwenda alikuwa akitumia "gia"
Ikabidi nitumie nguvu kubwa zaidi kuangalia kile "kirungu" au gia ni namna gani kinavyotumika.
Nilipoangalia kwa umakini sana pale juu ya kile kirungu niliona namba 1,2,3,4,5 na R.
Mwanzo wa safari yetu wakati tunaondoka pale stendi, Kile kirungu alikielekeza kwenye herufi R, nikaona gari ikirudi nyuma maana kuna gari nyingine iliyokuwa mbele yetu. Baada ya kurudi nyuma kidogo na palipopatikana upenyo wa ile gari yetu kupita, dereva alielekeza kile kirungu kwenye namba 1 hatimaye nikaona gari ikienda mbele.
Kadri tulivyoendelea mbele dereva alikuwa akihamisha kile kirungu kutoka namba hadi namba. Yaani alitoka 1 hadi 2 akaendelea 3,4 hadi 5. Sikumwona akitumia tena au akilekeza kile kirungu kwenye herufi R.
Hata wakati alipotaka kupakia barabarani sikumwona akirudisha kile kirungu kwenye herufi R, mara nyingi alikuwa akikiacha kikiwa katikati, na alipomaliza kupakia abiria alikielekeza kwenye namba 1 gari ikasonga mbele kwa mbele.
Baada ya kutumia muda mrefu saaana kumuangalia yule dereva, huku nikizalisha maswali mengi kichwani, nilishindwa kuvumilia ikabidi nimuulize yule dereva. Mbona huelekezi hicho kirungu kwenye hiyo herufi R? Mbona umekitumia mara moja tuu.
Ndipo akaniambia kuwa Hiyo herufi R ni gia ya kurudi nyuma, mara nyingi tunapoendesha gari gia hii huwa tunaitumia mara chache sana, haswa kwa biashara zetu hizi za kubeba abiria. Abiria wao wanaenda mbele, sasa tukiweka hii gia ya kurudi nyuma hawatafika na sisi hatutapata pesa, maana tutakuwa tunarudi nyuma tu, Wakati ananiambia maneno haya alikuwa akihama kutoka namba 3 hadi 4, huku gari ikizidi kuongeza mwendo tofauti na ule wa wakati ameweka namba1.
Nikamwambia ahsante kwa majibu yako. Lakini mbona ukihama kutoka namba 1 au 2 unapohamia 3 au 4 mwendo unaongezeka? Akaniambia siku zote unapoanza safari huwa ngumu sana au nzito lakini kadri unavyosonga mbele safari huwa nyepesi, hivyo ninavyobadili gia kutoka 1,2 kwenda 3 au 4 gari huwa nyepesi sana hivyo mwendo nao unaongezeka.
Kila alipozidi kubadili gia ndivyo ambavyo mwendo uliongezeka.
Nikamsikia "konda" akigonga bodi akiashiria kuwa ameona abiria anaetaka kuingia kwenye gari. Wakati huo dereva alikuwa kwenye gia namba 5, wakati anasimamisha gari alianza kurudi gia za nyuma yaani 4, 3, 2 hadi 1. Nilichoshangaa tena wakati anabadili gia hizi kurudi nyuma gari nayo ilikuwa ikipunguza mwendo.
Nilijifunza mambo mengi sana kuhusu mfumo huu unaotumiwa na gari hili.
Katika maisha yetu ni vyema tukajitengenezea mfumo kama wa gari. Unapoianza safari mara nyingi hurudi nyuma kuangalia mwanzo wako, Ni namna gani mbele yako kulikuwa na vikwazo vingi vinavyokuzuia wewe usisonge mbele, rudi nyuma mara moja tu, utengeneze mwanya wa wewe kusonga mbele. Yule dereva alirudi nyuma mara moja tu ili kukwepa ile gari iliyokuwa mbele yake.
Ni lazima ukubali kurudi nyuma mara moja tu, yule dereva angeng'ang'ania kuweka gia za mbele angeweza kusababisha ajali na safari yake ingekwama.
Unapoanza kusonga mbele, mara nyingi mwanzo huwa mzito. lakini kadri unavyozidi kubadili gia za kusonga mbele safari huwa nyepesi yale mazito uliyokuwa ukiyaona yanakuwa mepesi. Kadri unavyozidi kwenda mbele ndivyo ambavyo unazidi kutengeneza fursa nyingi zinazokuletea faida.
UKIRUDI NYUMA MARA MOJA SONGA MBELE MARA TANO ZAIDI
Usikubali kurudi nyuma mara nyingi. Ukiwa jeshini yule anayeonekana kurudi nyuma huwa anapigwa risasi. Kwenye daladala dereva akianza kuweka gia ya kurudi nyuma tu, hakuna abiria atakaepanda gari hiyo. Matokeo yake watakosa pesa.
Ukikubali au ukiruhusu kuwa mtu wa kurudi nyuma tu, jiandae kupigwa risasi, jiandae kukosa abiria, jiandae kukosa fursa.
Ukianza jambo jitahidi lisonge mbele na wala sio kurudi nyuma.
Insipired by Steven Mshiu.
+255 655 882074
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni