Jumatano, 6 Septemba 2017

NEVER LOOSE HOPE

USIPOTEZE TUMAINI KWA HARAKA.
Na Steven Mshiu.
Luka 7:18-23
Nimekutana na watu wengi wakiwa wamekata tamaa kabisa. Wamechoka kuishi hapa duniani. Wengine hudiriki kusema ni afadhali kuf kuliko kuendelea kuishi,
Hali ngumu ya maisha, majaribu, magonjwa, kukataliwa, na kila aina ya mateso vimekuwa ni vyanzo vikubwa vya wanadamu kupoteza tumaini kwa haraka.
Haijalishi kuwa utakuwa kwenye mazingira gani au wewe ni nani na umefanya nini, lakini tu pale unaporuhusu nafsi kupoteza tumaini hapo ndipo unapomruhusu shetani akutese sawasawa.
Alitokea mtu mmoja aliyezaliwa kwa ishara ya kimbingu, baba yake alikuwa ni kipofu(alikuwa na tatizo la kutoona). Katika harakati za kupewa jina kukaleta utata. Ndipo baba wa mtoto alipotaka aletewe kalamu na karatasi kisha akaandika jina la mwanae.
Mama wa mtoto huyu aliitwa Elizabeti na baba yake aliitwa Zakaria. Mtoto huyu alizaliwa siku zake zikiwa bado hazijatimia. Jina lake aliitwa YOHANA. Huyu ndiye Yohana aliyembatiza Yesu.
Ni nabii aliyetabiri kipindi cha Agano la kake na Agano jipya. Ni nabii aliyetabiri habari za Yesu na akamshuhudia Yesu. Ndiye aliyekuwa mtangulizi wa Yesu. Alitabiri kazi kubwa ambazo Yesu angekuja kuzifanya hapa duniani.
Injili yake ilikuwa ni ya upako sana. Alihubiri nyakati zote, Muda mwingi aliutumia kukaa nyikani akihubiri na kubatiza watu. Watu walitoka mjini na mijini na kumfuata kule nyikani ili kusikia habari za masihi atakaekuja.
Ikafika kipindi nabii huyu akaingia katika shida. Akapoteza tumaini juu ya Yesu aliyekuwa akizisema habari zake, Kwamba hata kamba za viatu vyake hataweza kuzilegeza. Akaamua kutuma wanafunzi wake waende kwa Yesu wamuulize je Ni yeye kweli au watazamie mwingine???
Yesu akawajibu wale wanafunzi, "nendeni mkamwambie mambo mliyoyaona, kuwa watu wanapona magonjwa yao, na misiba yao, pepo wabaya wanawatoka watu, vipofu wanaona, na mambo makubwa yanatokea"
Nina imani wanafunzi hawa wa Yohana walipofikisha habari hizi kwa Yohana, Tumaini lake lilirudi. Kipindi hiki Yohana alikuwa gerezani akisubiri kuuawa. Akahisi endapo atakufa je yale aliyoyatabiri ni kweli yatatukia?
TUNAJIFUNZA NINI LEO???
*Kuna wakati unafika tunatabiri mambo makubwa kutokea lakini ghafla tumaini la kuyaona yale mambo makubwa yakitokea linapotea ghafla. Hii inaweza kuchangiwa na hali ya kimaisha tunayopitia, au magonjwa au chochote kile.
*Ulikuwa n alengo la kusona uje kuwa mtu fulani, lakini kinainuka kikwazo cha kukosa ada. Kule kukosa ada kunakufanya upoteze tumaini la kutimiza ndoto yako ya kielimu. Leo nakuletea habari hizi kuwa mambo makubwa yanatendeka, Usipoteze tumaini kwa haraka. Nafasi yako bado ipo. Hakuna aliyeijaza bado inakusubiria wewe.
*Ulikuwa na mipango mingi baada ya kumaliza chuo lakini huu ni mwaka wa saba bado hujapata kazi. Umepoteza tumaini kabisa. Umejiona kuwa wewe ni wa kushindwa tu. Waliokuwa nyuma yako wana mafanikio makubwa. Lakini wewe bado upo katika hali ngumu. Leo nina ujumbe wa matumaini kuwa USIPOTEZE TUMAINI KWA HARAKA.
Kama ilivyo kwamba usiku hauwezi kuizuia asubuhi isifike, ndivyo ambavyo shida, magonjwa na hali unayopitia haitaweza kukuzuia kuifikia ndoto yako. Usipoteze Tumaini kwa Haraka.
Nataka nimtie moyo kijana na binti mmoja kuwa, umekuwa ukishuhudia kila jumamosi wenzako wakioa na kuolewa, lakini wewe hadi leo hakuna hata aliyekusemesha. Usipoteze tumaini kwa haraka. Hata wewe siku yako itafika. Jifunze kwa sara. Alimsubiri Isaka akampata akiwa na miaka tisini, ingawa alipoteza tumaini lakini bado alilirejesha tena.
*Tambua hila na mbinu za shetani. Kazi kubwa ya shetani ni kukufanya upoteze tumaini, maana anafahamu fika kuwa mtu mwenye tumaini hana hofu juu ya chochote. Mlango mkubwa shetani anaoutumia kumpata mtu ni kumwingizia hofu. Ukipatwa na hofu tu tumaini linayeyuka.
Niliwahi kukutana na mtu mmoja akinyunyiza sijui ni dawa gani katika eneo la nyumba yake, Nilipomuuliza kulikoni, Akaniambia kuwa amepewa dawa hiyo na "mtaalamu"
ili iwe kinga ya mji na nyumba yake dhidi ya wachawi. Nikatambua kuwa mtu huyu amepoteza tumaini.
Nikamshirikisha mtu mwingine juu ya biashara fulani niliyokuwa nimekusudia kuifanya. Akaniambia kabla kabla hujaanza twende nikupeleke mahali ukapatiwe kinga na dawa. Nikamjibu kuwa nina kinga moja tu ya Yesu nawe nikupe kinga hiyo. Hakuwahi kuwasiliana na mimi tangu siku hiyo.
Mpendwa huna haja ya kwenda kwa waganga, Huna haja ya kutafuta mazindiko kutoka kwa wachawi, Huna haja ya kuogopa majaribu, Huna haja ya kuogopa vikwazo unavyokutana navyo. Bado liko tumaini la kuinuka na kusonga mbele. Biblia yangu inaniambia mahali fulani kuwa kama liko tumaini kwa mti uliokatwa kuwa utachipua tena hata kwako yale mambo yanayoonekana kama yamekufa bado yatachipuka tena.
Bado hujachelewa
Usipoteze tumainikwa haraka.
Naamini nimezungumza na moyo wa mtu mmoja.
Kama ni wewe hebu sema neno moja kuwa
"NAREJESHA TENA TUMAINI LANGU"
Inspired by Steven Mshiu
0655 882074

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MAKUNDI MAWILI YA WATU WANAOKUZUNGUKA.

FAHAMU MAKUNDI MAWILI YA WATU KATIKA MAISHA YAKO. Na Steven Mshiu . Maisha ya kila mwanadamu yamezungukwa na watu. Watu hawa waweza kat...