Jumatano, 19 Aprili 2017

KULEWA MADARAKA.
Na, Steven Mshiu
Leo napenda tuangalie hili suala la madaraka. Madaraka ni mfumo wa Mungu mwenyewe aliounzisha huko mbinguni yeye mwenyewe. Mungu yeye mwenyewe mi mwenye madaraka na hufuata protoko yaani husimamia kanuni zake za kiuongozi na utawala.
Kiongozi yeyote anaesimama na kuliongoza taifa lolote, hupewa mamlaka na maongozi kutoka kwa Mungu. Hivyo ni vyema kuitii na kuiheshimu kila mamlaka iliyopo. Sisi hatuna mamlaka ya kumhukumu kiongozi yeyote anaesimama mbele yetu hata kama amekosea kiasi gani. Yupo Mungu aliemuweka ndiye anaeweza kumhukumu. Biblia inatuagiza hivyo.
Leo nataka nikuletee kisa kimoja cha mtu alieitwa Sauli. Sauli alichaguliwa na kutawazwa na Mungu ili awe mfalme juu ya taifa la Israel. Mtu huyu alitoka ktk jamii ndogo sana ya Israel yaani alikuwa ni jamaa ya Benyamini.
Baada ya wana wa Israel kukosa mfalme na mwamuzi juu yao kwa muda mrefu sana tangu kipindi cha Samsoni ndipo wakamwambia Samwel awatafutie mfalme atakaewaongoza ktk vita. Nyakati hizo taifa hili teule la Mungu lilikuwa limemsahau Mungu kabisa. Hawakutambua mamlaka na madaraka ya Mungu kuwa ni tofauti na ya dunia hii
Hawakukumbuka aliewaongoza jangwani pindi walipotoka Misri. Hivyo wakawa wanataka mfalme. Ndipo Mungu alipomwinua Sauli.
Baada ya Sauli kuinuliwa na kuwa mfalme juu ya Israel, akaota pembe. Akajisahau ya kwamba ametoka ktk jamii ndogo sana ya Benyamini. Akasahau kuwa alipakwa mafuta illi aliamue taifa teule la Mungu. Akaacha kumsikiliza mchungaji wake Samwel. Akajipa cheo cha Mungu. Akajiona kama yeye ni mungu wa israel. Akafanya kama alivyoweza.
Siku moja Bwana Mungu akampa Samweli maelekezo kuwa amwambie Sauli aende awapige Amaleki na kuharibu kabisa kila kitu cha hao Amaleki maana waliwatesa sana Israel walipokuwa wakitoka Misri. Tena asiache mfugo hata mmoja wa hawa Waamaleki.
Sauli hakutaka kuyasikia hayo maneno na maagizo ya Mungu kupitia kwa Samwel.
Sauli akatoka akaandaa jeshi kuishukia Amaleki. Akajifanya mwema sana. Akawaambia Wakeni waliokaa Amaleki kuwa waondoke asije akawaua pamoja na Amaleki. Akaanza kuipiga Amaleki. Akawaona kondoo na ng'ombe walionona akawaacha. Akamkamata mfalme Agagi, mfalme wa Waamaleki na kumwacha hai.
Lakini mtu huyu alipewa maagizo kuwa asiache kitu hata kidogo. Wala hakuyatii maagizo hayo. Akafanya kwa maamuzi yake.
Mungu akanena na Samweli kwa mara nyingine kuwa anajuta kwa sababu alimtawaza ili awe mfalme maana amerudi nyuma wala asimfute Mungu. Wala hakufanya yale aliyomwamuru. Kwa hiyo Mungu akamkataa kabisa Sauli. Ni kwa sababu alilewa madaraka.
Sauli alipoulizwa kwanini hakutii maagizo ya Mungu, yeye alijitetea kuwa ametii na amewachukua hao wanyama ili waje kumtolea Mungu sadaka. Mara ni wale watu ndio waliowaacha hao kondoo. Yeye hakusimama ktk nafasi yake. Hakuambiwa amwache Agagi akiwa hai. Hili likawa ni kosa kubwa sana mbele za Mungu.
Hivyo Mungu akamwacha Sauli kabisa. Tena akamkataa. Yote haya ni kwa sababu alilewa madaraka.
Siku za leo kuna watu ambao Mungu amewadhamini na kuwapa kanafasi kadogo tu ka uongozi lakini wanautumia vibaya. Kumbuka uko kwa niaba ya Mungu. Tumia mamlaka yako vizuri. Watendee wananchi haki. Tafuta kuyafuata maagizo ya Mungu. Viongozi wa dini wana nafasi kubwa sana ktk nafasi yako ya uongozi. Ni vyema kuwasikiliza. Wao ni sauti ya Mungu. Wao ndio kina Samwel wa leo. Ndipo utakapoona mafanikio makubwa ktk mamlaka uliyopewa.
Kisa hiki sio mimi niliyetunga. Ni maandiko halisi kutoka katika Biblia. Kisa hiki kwa wale wasomaji wa Biblia kinapatikana ktk kitabu cha 1 Samwel 15:1-34.
Tumia nafasi unayoipata kwa umakini.
Mungu akubariki sana.
0655 882074
DHAMBI INA ASILI YA UPOFU.
Na Steven Mshiu.
Nakusalimu kupitia jina la Kristo Yesu. Ni siku nyingine tunapoianza wiki ambayo naamini itakuwa ya baraka sana kwako.
Kila siku tunajifunza na tutaendelea kujifunza maadam bado tupo hapa duniani hivyo ni lazima tujifunze.
Wakati fulani nikawa najiuliza inakuwaje hadi mtu anajikuta anatenda dhambi? Je hajui madhara ya dhambi? Kwamba dhambi inaondoa utukufu wa Mungu? Dhambi inasababisha ubaki uchi? Dhambi inakufanya wewe kuwa mtumwa? Licha ya kujua mambo yoooote hayo lakini wanadamu tunajikuta tumeshatenda dhambi. Kwanini? Dhambi ina asili ya upofu.
Jana wakati nafundisha somo la asubuhi kanisani kwetu katika kipindi cha UANAFUNZI NA MAANDIKO katika mafafanuzi yangu ndipo nilipoweza kupata majibu ya maswali niliyokuwa nikijiuliza. KWanini mtu anafahamu fika madhara ya dhambi lakini bado anatenda dhambi. Dhambi ina asili ya upofu.
Katika historia ya wana wa Israel, Mungu alikuwa akiwapiga na kuwaadhibu sana kwa sababu ya makosa ya kujirudia rudia. Kosa lao kubwa ni walishindwa kumtegemea na kumwamini Mungu. Mara nyingi walimwacha Mungu na kutegemea akili zao. Kipindi fulani wakiwa pale jangwani walianza kumlalamikia Musa kuwa aliwatoa Misri ili waje kufia pale jangwani. Hawakuona ule utmwa wa zaidi ya miaka 430 kule Misri. Hawakukumbuka jinsi Mungu aliliangamiza jeshi lote la Farao mbele ya macho yao. Kwanini? Dhambi ina asili ya upofu.
Pale walipotubu na kuomba rehema Mungu aliwarehemu. Pale walipopata ka ahueni kidogo wakajisahau tena. Unajua mwanadamu anapopata mafanikio kidogo mara nyingi humsahau Mungu. Wakati ambao mwanadamu anapopitia changamoto fulani huwa ni wakati wake wa kuwa karibu na Mungu sana. Lakini ile changamoto inapoisha hufikiri labda ni kwa sababu ya uwezo wake.
Baada ya taifa la Israel kupitia mateso mengi ikiwa ni katika utawala wa kuhani Eli na watoto wake ambao hawakutaka kuishi sawa na mapenzi ya Mungu. Hawakutaka kumsikiliza Mungu. Mungu akamwinua Samwel kuwa mwmuzi juu ya taifa hilo. Samweli akafanya kazi ya kuurudisha ule uwepo wa Mungu uliokuwa umeondoka. Akafanya maombi ya toba na rehema. Taifa la Israel likawa ktk raha kubwa ktk kipindi cha uamuzi wa Samwel. Mungu akapigana kwa ajili yao. Adui zao walipojipanga juu yao, Mungu aliwapiga kwa mvua ya mawe. Dhambi ina asili ya upofu.
Baada ya kukaa kwa raha muda mrefu kwny kipindi hiki cha Samwel. Ikumbukwe hapakuwa na mfalme. Kwani Mungu ndie aliekuwa mfalme. Israel wakaanza kutafuta sababu ya kumtenda Mungu dhambi. Wakamwendea Samwel wakitaka awafanyie mfalme ili wafanane na mataifa mengne.
Ili mtu atende dhambi huanza kuwa sababu zisizo na mashiko. Hawa wazee wanamwambia Samwel kwamba yeye amekuwa mzee na wanawe hawaendi ktk njia zake lakini lengo lao ni kumkataa Mungu kuwa mfalme wao. Wanataka mfalme atakaewaongoza ktk vita ili wafanane na mataifa mengine.
Ingawa Samwel aliwaambia mfalme wanaomtaka atakuwaje kwamba atawatumikisha, atawatesa, ataweka kodi kubwa, wao hawakusikia bali waliendelea kudai mfalme ili wafanane na mataifa mengine.
Hapa tayari walishatoka ktk mpango wa Mungu. Wanataka kufuata desturi za kidunia. Hawakukumbuka kuwa baba zao walipigwa kwa sababu hizo. Dhambi ina asili ya upofu.
Mtu mmoja akawa anafahamu fika kuwa kujenga nyumba juu ya mchanga ni lazima izolewe na mafuriko, lakini anajenga tu. Watu wanapomshauri kuwa asifanye hivyo yeye yuko bize kujenga. Matokeo yake anakuja kupata hasara kubwa zaidi.
Kijana leo unashauriwa usifanye hivi n kwa sababu dhambi imeshakupofusha unaendelea tu. Matokeo yake unakuja kufa kwa ukimwi. Wewe binti unashauriwa usicheze cheze na vijana kwanza ndo uko kidato cha tatu. Unafahamu fika unaweza kupata mimba, kwa sababu dhambi imekupofusha unaenda tu, mnakubaliana, mnafanya yenu, unapata mimba labda na ukimwi juu. Lakini tokea mwanzo ulifahamu madhara yake. Mwisho unajikuta ukiwa ktk hali mbaya zaidi.
Zipo dalili kadhaa zinazoonyesha kuwa mtu anakaribia kutenda dhambi.
• Kutotaka ushauri. Ukiona mtu hataki kushauriwa au hachukui hatua yeyote ile pindi anaposhauriwa hapo amefikia hatua mbaya zaidi ya kuangukia kwny dhambi.
• Kutafuta sababu. Ukiona mtu anatoa visababu sababu katka kumtumikia Mungu yupo kwenye hatari zaidi. Muda wa ibaada unapofika unaanza kutoa visababu vinavyokufanya usiende ibadani upo kwny hatari. Kilichowaponza Israel ni mambo kama haya haya.
• Kutaka kufanana na wengine. Mtu anapookoka huwa anabadilishwa moja kwa moja. Anakuwa milki y Mungu sasa anapotaka kufanana na wengine, hali hii husababisha nguvu zetu za kiroho kupotea.
Ukisoma katika kitabu cha 1 Samwel 8:1-22, ndipo utakutana na kisa hiki cha ajabu sana jinsi gani hawa watu walidhamiria kumkosea Mungu ingawa walishauriwa ila kwa sababu dhambi imeshawapofusha hawakuweza kubadilika.
Mpendwa mtu wa Mungu epuka kuwa mtumwa wa dhambi. Dhambi inakufanya uendelee kuumia na kuwa mtumwa.
Tubu leo na ukubali kubadilika.
Ubarikiwe.
©Steven Mshiu
0655-882074

Kuokolewa kwa Neema

KUOKOLEWA KWA NEEMA.
Na, Steven Mshiu.
Wokovu wa mwanadamu ulianza kuandaliwa na MUNGU mwenyewe mapema pale bustanini Eden mara baada tu ya mwanadamu kumtenda Mungu dhambi na kuondoka katika uwepo wa Mungu.
Baada ya daraja la mawasiliano baina ya mwanadamu na Mungu kuvunjika, michakato mbalimbali iliweza kufanyika ilhali tu mwanadamu aweze kurudi katika mstari.
Mwanzo kabisa Mungu anamkamata mnyama asiyekuwa na hatia hata kidogo. Akamchinja ili kuwapatia wanadamu mavazi yatakayoficha ule utupu wao. Kumbuka dhambi inamfanya mtu kuwa mtupu yaani uchi. Unajua wokovu umetufunika. Yaani kuna mambo au vitu ambavyo vinatufanya tusionekane safi mbele za Mungu, hivyo kupitia wokovu ambao uligharimu uhai wa kitu umeweza kututakasa.
Lakini damu na ngozi ya yule mnyama havikuweza kukidhi mahitaji ya wokovu wa mwanadamu. Yote haya yalitokea katika Agano la Kale. Mungu alikuwa akiwapatia wokovu kupitia damu za wanyama.
Baada ya mambo yote haya, alitakiwa mtu atakae kuwa tayari kuyatoa maisha yake na uhai wake kwa ajili ya wanadamu na sifa za mtu huyo ni lazima awe mtu asye na hatia, mwenye upendo na atakaekubali kufa. Tena kifo cha msalaba.
hapakuonekana kiumbe chochote kile chenye uhai, mbinguni wala duniani kilichoweza kusimama na kusema kuwa atajitoa kwa ajili ya kuwakomboa wanadamu. Ukimya mkubwa ukatanda mbinguni.
Katika Ukimya ndipo alipojitokeza mtu mmoja akasema kuwa yeye atakwenda kuyatoa maisha yake kwa ajili ya wanadamu, ili kupitia damu yake wanadamu tupate wokovu
Huyu ni YESU KRISTO mwana wa mfalme MUNGU. Hakuona kule kuwa mwana wa Mungu kuna thamani kuliko mwanadamu alieumbwa kwa mfano wa Mungu.
Hivyo akayatoa maisha yake kwa ajili ya kuwaokoa wanadamu.
Kwa sababu hiyo basi nakusudia kuanza kuandika kitabu kinachohusu "MAMBO TISA YANAYOKAMILISHA WOKOVU".
Nitafurahi sana kupata mchango wako na mawazo yako ili kuweza kukifanya kitabu hicho kuwa bora zaidi. Najua sote tunatamani kuufahamu wokovu wetu na gharama zake ili tuweze kufika mbinguni.
Kama utakuwa na mchango wowote tafadhali waweza kunitumia ktk inbox yangu ya Facebook, au kupitia E-mail smshiu42@gmail.com
Au kupitia simu ya mkononi namba 0655-882074 na 0768-882074
Naamini tutashirikiana vyema katika kuujenga mwili wa Kristo.
Mungu akubariki sana.
SIRI TATU ZINAZOWEZA KULETA USHINDI MKUBWA.
--------------------------------------------------------------------------
Na, Steven Mshiu.
Shalom mtu mwema sana wa Mungu. Naamini umekuwa na wakati mwema wa mapumziko mazuri ya kuikumbuka pasaka ambayo Yesu alitolewa au alijitoa kwa ushindi mkubwa ili kuleta ukombombozi wa mwanadamu.
Tunapoadhimisha siku hii tukumbuke kuwa Yesu yu karibu kurudi kulichukua kanisa au wale watakaokuwa na alama ya damu ya Yesu ktk mioyo yao. Damu iliyotuletea wokovu mkuu sana.
Jana niliweza kupata fursa na kibali cha kufundisha Neno la Mungu katika kanisani, hapa moshi-Mdawi, na niliweza kushirikiana ujumbe huu ambao ulikuwa baraka sana kwangu binafsi na hata kwa washirika wote.
Hivyo nimeona ni vyema nikakushirikisha nawe japo kwa kidogo tu.
Unafahamu kuwa hakuna ushindi unaopatikana kimiujiza ujiza. Hakuna ushindi unaotokea from nowhere. Ushindi unapatikana kwa kuvuja jasho, tena baada ya maumivu makubwa sana.
Matokeo ya ushindi ni kutuzwa. ILi mshindani aweze kutuzwa ni lazima ahakikishe anapambana hadi mwisho wa mchezo. Huwezi kuishia katikati ya mchezo halafu ukategemea kupewa zawadi. Hiyo itakuwa ni ndoto.
Yapo mambo mengi yanayoweza kuwa sababu ya kukuletea ushindi mkubwa sana, lakini kwa leo nataka nikuletee mambo haya matatu ambayo yamekuwa ni siri kubwa na yenye mafaniko kwa washindani.
#SiriYaKwanza.
UJASIRI. Unapoingia katika mashindano yoyote yale jambo la kwanza unalotakiwa kufanya ni kujivika ujasiri. Ujasiri ni kile kitendo cha kufanya jambo pasipo kuwa na woga, pasipo kuwa na hofu. Huku ukitarajia kuwa kuna matokeo mazuri yatakayotokea juu ya kile unachokifanya. Ujasiri unakupa uwezo wa kujiamini.
Ujasiri unakufanya umuone mshindani wako kuwa hana uwezo kama wako. Kwa wale mashabiki wa mpira wanaweza kukubaliana nami, maana timu zinapoingia uwanjani huingia kwa ujasiri mkubwa sana huku kila timu ikiamini kuwa ni lazima ishinde.
Kifo cha msalaba kilihitaji mtu jasiri. Mtu atakaekubali kudharauliwa na kuaibishwa kwa ajili ya makosa ya wanadamu. UJASIRI ndio kitu pekee kilichoweza kumfanya YESU aiistahimili hukumu ya kifo cha msalaba. Kitu kinachohafifisha Ujasiri ni maneno ya watu. Dharau kutoka kwa wanaokuzunguka. Unaweza ukapanga kufanya jambo fulani either biashara, lakini watu wanapoanza kukubeza na kukudharau ile hali ya kuthubutu inapotea na hatimaye unaingia katika hatari ya kulipoteza lengo na kusudi la wewe kuishi hapa duniani.
#SiriYaPili. KUSUDI KAMILI.
Hakuna mwanadamu aliezaliwa kwa bahati mbaya. Kila mwanadamu yupo hapa duniani kwa kusudi maalum. Katika dunia hii ya sasa yenye ushindani mkubwa kila nyanja inahitaji watu wenye kulitumika kusudi lao la kuwepo hai hadi wakati huu. Unapolitambua kusudi kamili ni lazima mabadiliko yatokee. Yesu alilitambua kusudi lake la kuja hapa duniani baada ya kuacha kila kitu huko mbinguni. Kusudi kuu lilikuwa ni kumwokoa na kumkomboa mwanadamu. Na hakukubali kuondoka hapa duniani kabla ya kulitimiza kusudi hilo.
Nawe pia unalo kusudi. Je utaondoka hapa duniani kabla hujalitimiza? Kumbuka kusudi kubwa la kuokolewa kwetu ni ili tumtumikie Mungu kama Yesu anavyotuagiza ktk Mathayo 28:18-20.
Baada ya utumishi huo thawabu yake inapatikana ktk Yohana 14 na 15. Mpendwa litumike kusudi hili. Tupo kwenye mashindano. Mpambano wetu ni juu ya shetani anaeibeza kazi ya msalaba. Ni lazima tupambane na tuhakikishe tunamshinda. Na tutapambana nae kwa kuitangaza habari Ya Msalaba. Habari za mshindi Yesu. Kwa kuwa Yesu alishinda Nasi tutashinda tu. KUSUDI KAMILI.
#SiriYaTatu. IMANI
Imani ni jambo kubwa sana na ni kitu cha muhimu kwa mwanadamu yeyote. Kila jambo linalofanyika na kuleta matokeo makubwa huanza kwa imani. Mkulima analima shamba, hakuna dalili yeyote ile ya mvua. Anaotesha mbegu ardhini tena kwenye vumbi. Imani yake kubwa ni kwamba mvua itanyesha na zile mbegu zitaoza na kuota na hatimae kuleta mavuno mengi. Mtu anaanza biashara kwa mtaji wa 50,000/= lakini anaamini kuwa kuna siku mtaji wake utakuwa mkubwa naatamiliki biashara kubwa. Tunawasiliana Na Mungu kupitia maombi ya imani. Imani anatufanya tuamini kuwa Mungu yupo. Tunaokolewa kwa imani tu, Imani yetu inatufanya tukubaliane na yale yote aliyotuagiza Yesu. Tunaamini kuwa kuna Makao ambayo yameandaliwa huko mbinguni kwa wale watakaoshinda. Imani Imani Imani.
Yonathani mtoto wa Mfalme Sauli alitumia siri hizi katika kitabu cha 1 Samwel 14:1-16. Aliweza kuwaletea Israeli ushindi mkubwa sana.
Jambo la msingi ni kuamini kuwa Mungu yupo pamoja nawe kwa kila unalolifanya kwa ajili ya kulitimiza kusudi. Na yuko tayari kukupatia ushindi mkubwa sana utakaokuwa historia kwa wale wanaokubeza.
Mungu akubariki sana.
(kesho nitakuletea sababu zinaokwamisha au kuchelewesha ushindi na namna ya kuzishinda)
@Steven Mshiu.
0655-882074
smshiu42@gmail.com

MAKUNDI MAWILI YA WATU WANAOKUZUNGUKA.

FAHAMU MAKUNDI MAWILI YA WATU KATIKA MAISHA YAKO. Na Steven Mshiu . Maisha ya kila mwanadamu yamezungukwa na watu. Watu hawa waweza kat...